Pages


Home » » WATOTO WANUSURIKA KIFO BAADA YA MAMA YAO KUPEWA TARAKA.

WATOTO WANUSURIKA KIFO BAADA YA MAMA YAO KUPEWA TARAKA.

Kamanga na Matukio | 06:15 | 0 comments
Baada ya Mama yao Bi Madawa kupewa taraka na mmewe, alichanganyikiwa hali iliyopelekea kuwatumbukiza shimoni watoto hawa na kutaka kuwanyonga, ndipo wasamalia wema walipofanikiwa kuwaokoa na sasa wanatunzwa katika mtaa wa Senjele, kwa Mwenyekiti wa mtaa Bwana Elieza Mtindi hivyo wasamalia wema wanaombwa mchango wa hali na mali ili watoto hao kuweza kujikimu na kuenda shule kwani mama yao amelazwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya katika Wadi ya wagonjwa wa akili.

Aliyembeba mtoto anaitwa Valena Jumanne mwenye umri wa miaka saba, aliyebebwa anaitwa Exaud Smith umri wa mwaka mmoja na kushoto anitwa Siri Smith umri wa miaka minne. Mchango wowote wasiliana na mmiliki wa mtandao huu kwa simu namba 0754 490 752 ili kukufikisha walipo ili kuweza kuokoa maisha ya watoto hawa.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger