Pages


Home » » WAKAZI WA MWAKIBETE JIJINI MBEYA WALIA NA WANAOTUPA TAKA ENEO LISILO RASMI.

WAKAZI WA MWAKIBETE JIJINI MBEYA WALIA NA WANAOTUPA TAKA ENEO LISILO RASMI.

Kamanga na Matukio | 05:43 | 0 comments
Na mwandishi wetu.
Wakazi wa mtaa wa Nyibuko kata ya Mwakibete wamewalalamikia baadhi ya wakazi wa maeneo ya jirani kwa kitendo cha kutupa taka eneo lisilo rasmi.

Wakiongea na mwandishi wetu kwa nyakati tofauti bwana Abasi Kalinga na Bi Albina Masheta wamesema kuwa licha ya kukatazwa kutupa taka eneo hilo watu hao wanaendelea kutupa taka hizo hasa nyakati za usiku .

Kwa upande wake afisa mtendaji wa mtaa huo ambaye hakutaka jina lake litajwe kwa sababu maalum amesema kuwa huwa wanafanya mikutano kila wakati kuzungumzia mazingira yao na kwamba waliweka vibao vya matangazo kuwataka watu kuacha kutupa taka katika eneo hilo.

Pia ameongeza kuwa wanampango wa kumtafuta mgabo wa kulinda eneo hilo ili waweze kuwakamata watu hao na kuwafikisha mbele ya sheria.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger