Pages


Home » » UJENZI WA SOKO LA SIDO MWANJELWA WAANZA KWA KUJENGA VIBANDA

UJENZI WA SOKO LA SIDO MWANJELWA WAANZA KWA KUJENGA VIBANDA

Kamanga na Matukio | 06:02 | 0 comments

Mkuu wa wilaya ya Mbeya Bwana Evans Balama.
+++++
Na mwandishi wetu.
Waathirika wa moto soko la Sido Mwanjelwa wameanza kujenga vibanda vya biashara zao upya baada ya Serikali kuwataka wafanyabiashara hao kuendelea na shughuli zao katika eneo hilo.

Akitangaza uamuzi wa Serikali kwa wafanyabiashara hao mkuu wa wilaya wa Mbeya Evanve Balama amesema wakati ujenzi wa soko la Mwanjelwa ukiendelea wafanyabiashara waliounguliwa vibanda vyao wanatakiwa kuanza ujenzi upya ili waweze kuendelea na shughuli zao.

Kwa upande wake katibu msaidizi wa soko la Mwanjelwa Sido Alanusi Ngongwe ametoa pongezi kwa Serikali kwa kuchukua uamuzi wa haraka kuwawezesha wafanyabiashara kuendelea na shughuli zao katika eneo ambalo limezoeleka kwa biashara.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger