Pages


Home » » RC MBEYA AWATAKA MAAFISA ELIMU, KUHAKIKISHA WALIMU KWENDA MASOMONI KWA AWAMU.

RC MBEYA AWATAKA MAAFISA ELIMU, KUHAKIKISHA WALIMU KWENDA MASOMONI KWA AWAMU.

Kamanga na Matukio | 01:38 | 0 comments

Habari na mwandishi wetu.
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abasi Kandoro amewataka maafisa elimu wa shule za msingi na Sekondari kuhakikisha wanaandaa mpangilio maalumu utakao wawezesha walimu kwenda masomoni kwa awamu.

Ametoa agizo hilo baada ya kuwepo kwa upungufu mkubwa ya waalimu waalimu katika shule za msingi na sekondari ambao unachangiwa na idadi kubwa ya waalimu kwenda masomo bila ya mpangilio.

Amesema taarifa ya waalim 6 kati ya kumi wa shule moja kupewa ruhusu ya kwenda masomoni imechangia kwa kiasi kikibwa kuongeza upungufu wa waalimu.

Wakati huohuo amewataka viongozi wa kisiasa na wazazi kushirikiana kujenga nyumba za waalimu na kuongeza kuwa uwepo wa waalimu jirani na maeneo ya shule husaidia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya shule elimu kwa wanafunzi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger