Pages


Home » » KATIBU TAWALA MKOA WA MBEYA BI SWAI AWATAKA WANAWAKE KUFANYA KAZI KWA BIDII.

KATIBU TAWALA MKOA WA MBEYA BI SWAI AWATAKA WANAWAKE KUFANYA KAZI KWA BIDII.

Kamanga na Matukio | 04:41 | 0 comments
 Mgeni Rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya Bi. Betha Swai akiwahutubia wanawake pamoja na wananchi walio fika katika Sherehe za kuazimisha siku ya wanawake Duniani Jijini Mbeya, katika viwanja vya Luanda Nzovwe.
 Afisa Maendeleo Jamii Mkoa wa Mbeya Bi. Stella Kategile akisoma risala ya kuazimisha siku ya wanawake Duniani jijini Mbeya.
 Mwenyekiti  wa Sherehe hizo Bi.Mary Tolemi akitoa Taarifa kwa Mgeni Rasmi .
 Baadhi ya vikundi vya kina mama vya Vikoba Jijini Mbeya. (Picha zote na Mbeya Yetu Blog)
*********
Habari na Mwandishi wetu.
Katibu tawala mkoa wa Mbeya Beatha Swai amewataka wanawake kufanya kazi kwa bidii ili waweze kuondokana na wimbi la umasikini ambalo limekuwa likiwakabilia hasa wanawake.

Ameyasema hayo leo kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake ambayo yameadhimishwa kiwilaya katika viwanja vya shule ya Msingi Ruanda Nzovwe huku kauli mbiu ya maadhimisho hayo ikiwa ni USHIRIKI WA MSICHANA UNACHOCHEA MAENDELEO”

Wakati huohuo Bi.Swai alitoa zawadi kwa wanafunzi watatu waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2011 ambao ni Feliste Silivesta kutoka Mbeya Sekondari, Jacklini Hindi kutoka Samora Sekondari na Grace Mikola kutoka Mbeya Sekondari.

Naye mwenyekiti wa kamati ya maadhimisho hayo Bi.Mery Gumbo amewataka wanawake kuwa wepesi kushirikiana kwa kujiunga kwenye vikundi vitakavyowawezesha kujipatia kipato.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger