Pages


Home » » ASHITAKIWA KWA WIZI - MBOZI

ASHITAKIWA KWA WIZI - MBOZI

Kamanga na Matukio | 04:29 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbozi.
Mwananchi mmoja Enn Sichone (22) mkazi wa Old Vwawa, Wilaya ya Mbozi, Mkoani Mbeya, amefikishwa mbele ya mahakama ya mwanzo kujibu shtaka la wizi.

Akisoma shtaka hilo mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo PC Lugano Mwampulule, mbele ya Hakimu mfawidhi wa mahakama ya mwanzo Ismael Karuta amesema mshtakiwa ametenda kosa hilo Machi 13 mwaka huu majira ya saa 12 kamili jioni.

Mtuhumiwa aliiba starter moja ya gari, radiator 2 za gari zinazomilikiwa na Bwana Said Salum wa Vwawa vyote vikiwa na thamani ya shilingi laki nane(800,000/=).

Hata hivyo mshtakiwa Enn amekana kutenda kosa hilo na keshi hiyo imeahirishwa hadi April 10 mwaka huu na hivyo kurejeshwa mahabusu kutokana na kukosa wadhamini.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger