Pages


Home » » BREAKING NEWS: MAUAJI, UCHOMAJI NYUMBA NA WIZI WA WATOTO.

BREAKING NEWS: MAUAJI, UCHOMAJI NYUMBA NA WIZI WA WATOTO.

Kamanga na Matukio | 05:14 | 0 comments
* KIJIJI CHA ISANSA WILAYA YA MBOZI MKOANI MBEYA.
Mgambo wamnyongwa mwananchi katika Ofisi ya Kijiji na kumbambikiza simu mfukoni mwake, marehemu afanyiwa uchunguzi na mtu asiye na sifa katika Zahanati ya Isansa wilaya ya Mbozi, ndugu wabaini alivutwa sehemu za siri hadi mauti yalipomfika. Ndugu wadai taarifa ya uchunguzi bila mafanikio.

* Mgambo wabomoa nyumba ya mwananchi na kuteketeza kwa moto na kuharibu pikipiki na kisha kumteka mke wa mlalamikaji toka Machi 15 mwaka huu na haifahamiki, alipo mpaka sasa. Vilevile mlalamikaji aishi uhamishoni kwa hofu ya kuuawa.

*Katika moja ya Hospitali zilizopo mkoani Mbeya yatuhumiwa kubadilisha watoto mapacha, ambapo mmoja wa mapacha alidaiwa kafariki lakini mapacha hao wakutana katika moja ya shuleni ya sekondari na vyeti vyote vinaonesha walizaliwa siku na muda mmoja na vipimo vya utambuzi vinasaba (DNA) vitabaini jumapili ya wiki hili Machi 25 mwaka huu.

Watoto hao wang'ang'ania kuishi pamoja babu yao akutanishwa nao abaini kuwa ni damu yao baada ya mizimu yao kupanda, mmoja kati ya wazazi adai kulipa gharama yoyote kumkomboa pacha mwenzie.

*****Kwa habari zaidi tembelea mtandao huu*****
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger