Pages


Home » » WAGANGA WA JADI WAPINGA VITENDO VYA UOVU JIJINI MBEYA

WAGANGA WA JADI WAPINGA VITENDO VYA UOVU JIJINI MBEYA

Kamanga na Matukio | 05:15 | 0 comments

Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
Waganga wa jadi na tiba asilia mkoani Mbeya  wamelitaka Jeshi la Polisi kutoa ushirikiano na watabibu wa asili  ili kukomesha vitendo  vya uovu  vinavyohusishwa na imani za kishirikina.

Hayo yamebainishwa na watabibu wa tiba asilia na tiba mbadala katika mkutano ulio fanyikia katika ukumbi wa Shamba la Bibi uliopo katika eneo la Sokomatora  Jijini Mbeya

Mwenyekiti wa mkutano huo Bwana Boniventura  Mwalongo uliohusisha vyama vya ATME, MJATA ,CHAWATATA , na CHAUMUTA vinavyohusika na tiba asilia hizo amesema tiba zao zimekuwa zikihusishwa na imani za kishirikina kwa kuchochea vitendo vya upigaji nondo, mauaji ya maalbino(walemavu wa ngozi) na ubakaji ambapo asasi hizo hazija kanusha hadharani kutokana na baadhi ya watu kuvamia fani hiyo kwa nia ya kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu.

Katika mkutano huo vyama hivyo vimeadhimia kupunguza vitendo vyote vya uovu vinavyofanywa na baadhi ya watu waliovamia fani hiyo kutoka nje ya nchi kwa kushirikiana na wa watanzania wasiosajiliwa wala kuwa na leseni ya kufanyia kazi hiyo.

Aidha wamelitaka Jeshi la Polisi kuwafichua hadharani wale wote wanaohusika na vitendo hivyo kwani wamekuwa wakifumbia macho licha ya kutajwa baadhi ya vigogo ambao ndio wenye mtandao huo.

Pia matabibu hao wa asili wamepiga vita marufuku matangazo yote ambayo hayana stahara katika vituo vya redio na matangazo yote yanayotoa matangazo yote yanayotangaza kuondolewa mara moja.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger