Pages


Home » » Kufuatia Mgomo Wa Madaktari Nchini,Serikali Yawasimamisha Kazi Katibu Mkuu Wizara Ya Afya Bi Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali Deo Mtasiwa.

Kufuatia Mgomo Wa Madaktari Nchini,Serikali Yawasimamisha Kazi Katibu Mkuu Wizara Ya Afya Bi Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali Deo Mtasiwa.

Kamanga na Matukio | 04:54 | 0 comments
Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Bi Blandina Nyoni

 Mganga Mkuu wa Serikali Bw Deo Mtasiwa.(Picha na 
Fununu Habari).
 
 
*********
Serikali imewasimamisha kazi katibu mkuu wa Wizara ya afya na ustawi wa jamii Brandina Nyoni na  mganga mkuu wa Serikali Dokta Deo Mtasiwa  ili kupisha uchunguzi wa vyombo vya dola juu  ya tuhuma zinazowakabilia kuhusu mgomo wa madaktari unaoendelea hapa nchini.

Uamuzi huo umetolewa na waziri mkuu Mizengo Pinda wakati akizungumza na madaktari jijini Dar es salaam katika kutafuta suluhu ya mgomo.

Aidha amesema Mawaziri wanaodaiwa kuhusika na tuhuma za kusababisha mgomo huo watasubiri maamuzi ya Rais, pia amesema Serikali imeongeza posho ya madaktari wanaoitwa kwa ajili ya matibabu ya dharula kutoka shilingi elfu kumi hadi kufikia shilingi elfu ishirini na tano.

Kutokana na ongezeko hilo sasa Serikali itatumia zaidi ya shilingi bilioni 210 kabLa ya bajeti ya serikali ya mwaka 2012/2013

Hata hivyo Serikali imeunda kamati ya kushughulikia maadhimio nane yaliyowasirishwa katika mkutano huo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger