Pages


Home » » MBABE WA KIJIJI AUAWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI - MBEYA

MBABE WA KIJIJI AUAWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI - MBEYA

Kamanga na Matukio | 03:42 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mtu mmoja maefariki dunai mkoani Mbeya baada ya kupingwa na wananchi wenye hasira kali wakimtuhumu kuwanyanyasa wananchi wa kijiji cha Halambo Kata ya Halungu wilaya ya Mbozi mkoani hapa.

Tukio hilo limetokea kijijini hapo ambapo wananchi hao walimpiga hadi kumuua mkazi huyo aliyefahamika kwa jina la Imani Msinjili (23), kwa madai kuwa marehemu akilewa huwapiga wananchi hao na kuwaletea vurugu kubwa hali waliiona ni bughudha kwao.

Imeelezwa kuwa majira ya saa tano asubuhi marehemu Msinjili alikuwa amelewa na kisha kuwapiga baadhi ya wananchi ndipo walipomkamata na kuanza kumpiga mpaka pale mauti yake yalipomfika katika eneo hilo la kilabu cha pombe alipokuwa marehemu akinywa.

Hata hivyo Jeshi la Polisi halikuweza kufika eneo la tukio mpaka jana Februari 23, mwaka licha ya kupewa taarifa na maiti iliendelea kuwepoeneo hilo.

Mwandishi wetu alipofanya jitihada za kumtafuta Kamanda wa Jeshi la Polisi Advocate Nyombi ili aweze kuthibitisha taarifa za tukio hilo hakuweza kupatikana mara moja.

Aidha kumekuwepo na tabia za baadhi ya wananchi mkoani hapa kuendelea na tabia za kujichukulia sheria mkononi licha ya Jeshi la Polisi na Viongozi wa madhehebu mbalimbali kuendelea kukemea vitendo hivyo viovu vinavyokiuka haki za binadamu.

Wakati huohuo wafanyabiashara wa Kijiji cha Mlowo bado wameendelea na mgomo wa kutolipa ushuru wa biashara na mazao wakidai wanahitaji kuonana na Mkuu wa wilaya ya Mbozi Mheshimiwa Gabriel Kimoro.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger