Pages


Home » » WANAKIJIJI WATIMUA AFISA MTENDAJI WA KAJIJI WAMKAIMIASHA MWANAKIJIJI.

WANAKIJIJI WATIMUA AFISA MTENDAJI WA KAJIJI WAMKAIMIASHA MWANAKIJIJI.

Kamanga na Matukio | 01:36 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Katika hali isiyo ya kawaida wakazi wa kijiji cha Matamba kata ya Isange wilayani Rungwe mkoani Mbeya wamemfukuza kazi afisa mtendaji wa kijiji hicho na kumpachika madaraka mwananchi wa kawaida kushika wadhifa huo.

Uamuzi huo umefikiwa jana wakati wa kikao cha kijiji kilichoketi kujadili hali ya maendeleo ya kijiji hicho ambapo, ilibainika kuwa afisa mtendaji alihusika na wizi wa shilingi milioni moja na laki sita, kujimilikisha saruji za wananchi zilinunuliwa kwa ajili wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya kata na kutumia vibaya madaraka.

Aidha wananchi hao walimchagua Fomen Mwandembo ambaye ni mwananchi wa kawaida kukaimu wadhifa huo hadi hapo Serikali itakapo mleta afisa mtendaji mwingine.

Mwenyekiti wa kijiji hicho John Mwakyoma amesema kuwa huamuzi huo hauwezi kupingwa kutokana na kwamba imekuwa ni tabia ya maafisa watendaji kujimilikisha mali za umma pasipo kuchukuliwa hatua zozote.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Isange Eliasi Mwasambili amesema kuwa baada ya tukio hilo walikubaliana kumwamisha kituo cha kazi afisa huyo badala ya kumfukuza.

Kwa mujibu wa sheria za nchi afisa mtendaji huajiliwa na hapatikani kwa njia ya uchaguzi, hivyo kitendo hicho ni kinyume na sheria na kanuni za utumishi wa umma.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Mwakyoma amesema anayabariki maamuzi ya wananchi kwani mtendaji huyo wamemuonya mara nyingi lakini lakini amekuwa akikaidi na kudhoofisha nguvu za wananchi na maendeleo kwa ujumla kijijini hapo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger