Pages


Home » » NDAMA (NG’OMBE) WA AJABU AZALIWA WILAYANI MBOZI. ANA MIGUU 6, MIDOMO 4 NA MACHO MATATU

NDAMA (NG’OMBE) WA AJABU AZALIWA WILAYANI MBOZI. ANA MIGUU 6, MIDOMO 4 NA MACHO MATATU

Kamanga na Matukio | 01:38 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
*Ana miguu sita, midomo minne na macho matatu

Ndama wa ajabu amezaliwa katika Kijiji cha Bara, Kata ya Bara Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya Aprili 19 mwaka huu.

Ndama huyo ambaye bado jinsia yake haijulikani ambapo mmiliki wake hakuwa tayari kutaja jina lake kwa masharti kwamba wazee wa kimila hawajampatia kibali cha kuzungumzia lolote kuhusiana na kiumbe hicho cha ajabu.

Aidha, ndama huyo ana jumla ya miguu sita, midomo minne na macho matatu lakini ana uwezo wa kunyonya kama kawaida.

Wazee wa kimila wa Kijiji hicho wamekuwa wakikutana mara kwa mara ili kupata mustakabali wa tukio la ajabu kijijini hapo.

Wakati wazee hao walikutana ndama huyo akiendelea vema na juhudi za kumtafuta Bwana mifugo wa Kata na Wilaya ya zinafanyika ili kujua sababu za ndama huyo kuzaliwa hivyo.
*****Endelea kutembelea mtandao huu na tutaelekea eneo la tukio kupata picha ya ndama huyo wa ajabu, mara ya kibali kutoka kwa wazee wa mila kukamilika******.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger