Pages


Home » » TUME YA MGOGORO WA ARDHI BAINA YA MWEKEZAJI WA KAPUNGA NA KIJIJI CHA MAPOGORO YAANZA KAZI.

TUME YA MGOGORO WA ARDHI BAINA YA MWEKEZAJI WA KAPUNGA NA KIJIJI CHA MAPOGORO YAANZA KAZI.

Kamanga na Matukio | 05:42 | 0 comments
Mfugaji Bwana Mungo Makubi (27) kushoto na Singu Mwakami (23) wakimtazama ng'ombe aliyeuawa kwa kugongwa na gari aina ya Toyota Landcruiser lenye nambari ya usajili T 566 BQH. iliyokuwa ikiendeshwa na mwekezaji wa Kapunga Rice Project wilayani Mbarali aitwaye Bwana Gerry Baquzein baada ya kuwakosa wafugaji hao baada ya kujistiri nyuma ya mti na kisha hasira za mwekezaji kuishia kwa kumgonga ng'ombe huyo mwenye thamani ya shilingi laki 6 za kitanzania na kisha kufa papo hapo. (Picha na Maktaba yetu).
*******
Habari Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Tume iliyoteuliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Abbas Kandoro, imeanza kazi ya kupima eneo la mipaka ili kujua uhalali wa pande hizo mbili zinazopingana kwa muda wa miaka sita sasa, ambapo kijiji hicho kimeshindwa kufanya shuguli za kimaendeleo kutokana na mwekezaji huyo (Kapunga Rice Project) kuwanyanyasa wananchi hao.

 Wakati tume hiyo ikiwa imeaanza kazi rasmi Aprili 19 mwaka huu, imeshuhudia mwekezaji huyo akibandika matangazo ya kuwataka wananchi wasipite maeneo kadhaa na kwamba atakamata mifugo, baiskeli, pikipiki, magari na waenda kwa miguu na kuwatoza faini watakapokiuka agizo hilo.

Amesema faini hizo zinaanzi shilingi 20,000 hadi 100,000 hali ambayo imepingwa na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bwana Ramadhan Nyoni pamoja na Halmashauri ya kijiji hicho na kuitaka tume hiyo ione yenyewe ukatili unaofanywa na mwekezaji huyo.

Aidha ni takribani miaka 6 mwekezaji huyo hajaweza kuendeleza kijiji hicho na kuhodhi shule, zahanati, miundo mbinu ya maji na umeme na hivyo kijiji hicho kuwa kama kisiwa na kuwafanya wananchi hao kuishi kama watumwa katika ardhi yao.

Baadhi ya wajumbe walioteuliwa katika Tume hiyo ya uchunguzi ni pamoja na Mwenyekiti Bi Frola Luvanda (Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda), Sospeter Kajuna (Afisa mipango Mkoa), Geofrey Mwaijobele (Afisa Mipango Wilaya ya Mbarali), Omary Mataka (Mpima Ardhi) na Enock Kyando (Afisa Mipango Mkoa).

Wengine ni Saimon Mlimandago na Clemence Mero ambapo tume hiyo itafanya kazi mpaka May 14 mwaka huu katika upimaji wa awali imeoneshwa na wananchi mipaka asili kabla ya kijiji hicho kulikabidhi Shirika na NAFCO ambalo lilipewa ardhi hiyo bure kwa ombi rasmi la Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, 1989 na kuanza rasmi mradi wa umwagiliaji 1993.

Hata hivyo uongozi wa Kijiji umeitaka tume hiyo kutenda haki ili kwani eneo waliloikabidhi NAFCO kipindi hicho ni hekari 5,500 badala ya 7,370 zinazodaiwa hivi sasa na mwekezaji kuwa ndizo alizouziwa ambapo hakunaukweli wowote na kijiji hicho kuonekana kipo ndani ya eneo la mwekezaji.

Wakati huo huo baadhi ya kare wanazozipata ni pamoja na kukamatwa mifugo na kuuawa, kuzuia kupitisha mazao kijijini hapo na mwekezaji huyo kushindwa kuyaendeleza mashamba hayo na kuwakodisha wananchi, kwa hiyo serikali iangalie upya kwani mwekezaji huyo hainufaishi Kijiji wala taifa.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger