Pages


Home » » AFARIKI BAADA YA KUNG’ATWA NA NYOKA.

AFARIKI BAADA YA KUNG’ATWA NA NYOKA.

Kamanga na Matukio | 05:02 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
Mkazi mmoja wa Narco, Kata ya Utengule Usangu Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Bi Gigwa Chelleh (16), amefariki dunia baada ya kung’atwa na nyoka mwenye sumu wakati akiwa shambani.

Tukio hilo limetokea Aprili 17 mwaka huu majira ya saa nane mchana, marehemu akiwa shambani baada ya kutumwa na mama yake Bi Digina Maleva kuchukua mboga kwa ajili ya kuwaandalia chakula nduguze waliokuwa machungoni.
Marehemu hakurejea mapema nyumbani hali iliyompelekea mama yake kuwauliza nduguze kuwa Gigwa mbona anachelewa kurudi, ndipo baadhi ya marafiki zake walipomjibu kuwa walimuacha marehemu akiendelea kuchuma mboga.
Baada ya kumfualia walimkuta marehemu amefariki huku mwili wake ukiwa umevimba na mguu wake wa kulia ukionesha kugongwa  na kitu kinachodhaniwa kuwa ni nyoka mwenye sumu kali na mwili ulikuwa umeharibiwa na sumu hiyo.
Aidha, mwili wa marehemu ulichukuliwa majira ya saa 11:30 jioni na kupelekwa katika Kituo cha Afya cha Igulusi, ambapo Daktari alibainisha kuwa marehemu amefariki baada ya kung’atwa na nyoka mwenye sumu.
Hata hivyo mazishi ya marehemu Gigwa yamefanyika Utengule Usangu Aprili 18 mwaka huu, na tunaiombea familia hiyo faraja katika kipindi hiki kigumu na roho ya marehemu ilale mahali pema peponi, Amina.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger