Pages


Home » » MVUA KUBWA ILIYONYEESHA WILAYA YA CHUNYA YAVUNJA NYUMBA 16 NA KANISA MOJA.

MVUA KUBWA ILIYONYEESHA WILAYA YA CHUNYA YAVUNJA NYUMBA 16 NA KANISA MOJA.

Kamanga na Matukio | 05:53 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Chunya.
Mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali imevunja nyumba kumi na sita na kanisa moja katika Kata ya Matundasi, Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya, Aprili 18 mwaka huu majira ya saa 10 kamili jioni.

Kanisa liliezuliwa paa kutokana na upepo huo la Kanisa la Tanzania  Assemblies of God (TAG) linaloongozwa na Mchungaji Mwanjoka, ambapo ukuta wa upande mmoja wapo ulivunjika na kuanguka hali iliyowasababishia waumini wa tano kujeruhiwa na kisha kukimbizwa katika Hospitali ya wilaya hiyo baada ya kufunikwa na kiusi cha ukuta.

 Waumini hao walikuwa katika shughuli za Ujenzi ambapo upepo mkali ulianguka ukuta na kusababisha mmadhara kwao, amjeruhi hao ni pamoja na Mama Mwashiwawa, Mama Doke na watoto watatu ambao majina yao hayakufahamika mara moja.

Baadhi ya wananchi waliathiriwa na janga hilo wamehifadhiwa na ndugu zao hivyo basi msaada wa karibu unahitajika ili kuwanusuru adha hiyo, kwani wanaupungufu wa chakula na malazi.

Wakati huo huo majeruhi wawili waliojeruhiwa katika sakata la Afisa Mtendaji wa kata hiyo Bwana Joseph Nangale kuhusishwa na ujambazi mwanzoni mwa mwezio huu, ambapo Bahati Sibonike alipingwa risasi miguu yote na Diki Lengai alijeruhiwa miguu yote kwa kupingwa na marugu kufuatia majambazi hao kuvunja duka la Bwna Hamis Choga na kupora milioni 24,300,000.

Sababu za kujeruhiwa kwao ni kutokana na kutoka kwenda kumsaidia Bwana Choga, ambapo Nangale alimpiga Lengai kwa kutumia marungu, hali iliyompelekea kupooza baadhi ya viuongo vyake na Sibonike amekatwa mguu mmoja.

Hata hivyo Afisa Mtendaji huo amekamatwa na Jeshi la Polisi na atafikishwa mahakamani wakati wowote kujibu mashtaka yanayomkabili.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger