Pages


Home » » SUNGUSUNGU WAMTIA ULEMAMVU MWANANCHI

SUNGUSUNGU WAMTIA ULEMAMVU MWANANCHI

Kamanga na Matukio | 05:42 | 0 comments

Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
Daudi Mwashitete (40) Mkazi wa Kitongoji cha Lunyego Kata ya Itaka, Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya amepata ulemavu baada ya kupingwa na sungusungu wa kijiji hicho, akidaiwa kuwa ni mwizi wa baiskeli.

Majeruhi huyo alikamatwa na sungusungu hao Aprili 8 mwaka 2011 katika Kijiji hicho akiwa na baiskeli yake, akidaiwa kuonyesha risiti ya baiskeli hiyo na yeye kudai kuwa ipo nyumbani kwake ndipo sungusungu hao walipoanza kumpiga kwa marungu yaliyowekwa misumali kisha kumpiga miguu yote miwili hali iliyompelekea kuvunjika.

Baada ya ukatili huo walimuacha na wao kuondoka na baiskeli yake na zoezi hilo lilisimamiwa na Afisa mtendaji wa kijiji cha Hangomba Bwana Watson Maduguli, ambaye kwa sasa ni Afisa mtendaji wa kijiji cha Bara, Kata ya Bata.

Bwana Mwashitete amepelekwa hospitalini ambapo madaktari walidai akatwe miguu kutokana na kujeruhiwa vibaya miguu hiyo, lakini alikataa na kukimbili kwa Mganga wa Kienyeji ambapo ametibiwa na hivi sasa anaendelea vema.

Aidha taarifa za kujeruhiwa kwake ziliripotiwa katika Kituo cha Polisi cha Itaka na sungusungu hao hawajachukuliwa hatua zozote licha ya Mkuu wa polisi wilaya ya Mbozi kupata taarifa.

Hata hivyo sungusungu hao wameendelea kufanya vitendo vya kikatili katika Kijiji kingine cha Bara, huku Mtendaji wa kata hiyo akifumbia macho na uongozi wa wilaya kutomchukulia hatua zozote pamoja na sungusungu.

Miongozi mwa sungusungu wanaolalamikiwa na wananchi hao ni pamoja na Iman Mdolo, Michael Mkondya, Wicref Mtambo na Malaso.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger