Pages


Home » » MWALIMU ALIYEWATAKA WANAFUNZI KIMAPENZI AFUKUZWA KAZI.

MWALIMU ALIYEWATAKA WANAFUNZI KIMAPENZI AFUKUZWA KAZI.

Kamanga na Matukio | 05:03 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
Aliyekuwa Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya Samaritan iliyopo mji mdogo wa Mbalizi, Mkoani Mbeya Mwalimu Francis Kita, amefukuzwa kazi baada ya kuwataka kimapenzi wanafunzi watatu wa Kidato cha tatu.

Mwalimu huyo aliyewataka kimapenzi wanafunzi hao kwa nyakati tofauti  alikiri kupokea barua ya kufukuzwa kazi lakini amekanusha kutenda kosa hilo.

Imedaiwa kuwa mwalimu Kita kwa kutumia madaraka na dhamana aliyopewa, alikiuka maadili ya taaluma ya ualimu baada ya kuwataka kimapenzi wanafunzi hao wawili(majina yamehifadhiwa), badala ya kuwafundisha au kuwajenga katika misingi ya kujisomea na malezi.

Hata hivyo mwalimu huyo alitaka kuitekeleza dhamira hiyo katika Ofisi ya shule hiyo kwa vile shule hiyo ni ya bweni, iliyopo nje yanjiji maarufu kama mji wa Mbalizi, Wilaya ya Mbeya Vijijini.

Baada ya wanafunzi hao kuona wanabugudhiwa waliamua kupeleka malalamiko yao kwa Mkuu wa shule Bi Faraja Mbwana, ambaye naye alitoa taarifa kwa Mkurugenzi wa shule hiyo Bwana Ben Mwasaka ambapo waliweka mtego wa kumnasa kirahisi mwalimu huyo ambaye anasoma pia Chuo Kikuu huria Jijini Mbeya.

Mwalimu huyo alipewa wadhifa huo hivi karibuni  na mara kwa mara amekuwa akilalamikiwa na baadhi ya wanafunzi ambao walidai kupewa adhabu pindi wanapokataa kwenda ofisini kwake.

Kwa upande wake Mkuu wa shule hiyo Bi Mbwana amesema kuwa ni kweli Makamu wake mwalimu Kita amefukuzwa kazi hivi karibuni, ingawa alisema kuwa msemaji mkuu ni Mkurugenzi wa shule hiyo Bwana Mwasaka.

Aidha Bwana Mwasaka hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo, kutokana na kuwa nje ya ofisi yake.

Uchunguzi umebaini kuwa Mkurugenzi huyo wa shule anampango wa kumburuza malimu huyo mahakamani kwa kitendo cha kuwadhalilisha watoto kuwalea kama mzazi.

Afisa Elimu wa Mkoa wa Mbeya Bwana Juma Kaponda amewapongeza watoto hao kwa ujasiri walioonesha na iwe mfano wa kuingwa ili kubaini vitendo viovu vinavyofanywa na walimu au watu waliopewa dhamana ya kuongoza.

Mbali na pongezi kwa wanafunzi hao pia ameupongeza uongozi wa shule hiyo kwa kuchukua hatua za haraka na makusudi, kutokana na uovu wanaofanyiwa watoto wa kike.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger