Pages


Home » » AUAWA BAADA YA KUPIGWA NA MCHI WA KUTWANGIA.

AUAWA BAADA YA KUPIGWA NA MCHI WA KUTWANGIA.

Kamanga na Matukio | 04:57 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linawatafuta watu watatu kwa kusababisha kifo cha mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Shinde Guda (33), huko Wilaya ya Chunya Mkoani hapa.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa Barakiel Masaki amesema marehemu huyo ni makazi wa Kitongoji cha Shinyanga, Kijiji cha Mamba B, Kata ya Lupa, Wilaya ya Chunya ambapo Aprili 22 mwaka huu majira ya saa tatu usiku marehemu alikuwa kuwa kilabuni na aliuawa kwa kupigwa na mchi kisongoni na watu watatu na kufariki papo hapo.

 

Masaki amewataja watuhumiwa hao wa mauji kuwa ni pamoja na Mashaka Chelehani (29), Emmanuel Mwalupembe (20) na Mengu Mwalupembe (18) ambao wote ni wakazi wa Lupa wilayani humo.

 

Hata hivyo watuhumiwa wote kwa pamoja walitoroka kusikojulikana mara baada ya kutenda tukio hilo.

 

Kaimu Kamanda huyo Barakiel amesema msako mkali unafanywa ili kuwakamata watuhumiwa na kwamba chanzo cha mauaji hayo ni ulevi kwani mara kadhaa walionekana katika hali ya kulewa.

Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger