Pages


Home » » MWANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE, APEWA MIMBA HALI ILIYOMSABABISHIA KUSHINDWA KUENDELEA NA MASOMO - MBEYA.

MWANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE, APEWA MIMBA HALI ILIYOMSABABISHIA KUSHINDWA KUENDELEA NA MASOMO - MBEYA.

Kamanga na Matukio | 05:55 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Iwalanje, Wilaya ya Mbeya Vijijini Mkoani Mbeya Pendo Jacob (17), amepoteza masomo baada ya kupewa mimba na Bwana Shungu Ringston Ndasoni (28), mkazi wa Kijiji cha Hatwelo, Kata ya Iwalanje.

Mwanafunzi huyo amefukuzwa shule hivi karibuni kufuatia wazazi wakeBwana Jacob Mwakambanga (60), na Bi Lomia Jacob miaka (30) kuitwa na Mkuu wa shule na kuambiwa kuwa binti yao ana ujauzito na miezi minne, baada ya kupimwa katika Zahanati ya kijiji hicho na kutakiwa kupeleka barua kwa Afisa Mtendaji wa kijiji ili tararibu za kumkata kijana aliyempa mimba binti huyo akamatwe.

Wazazi baada ya kupewa barua hiyo walikwenda kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji Bwana Rafael Mwandoje pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji Ibrahimu Mponzi, ambao walimuita mtuhumiwa na wazazi wake na kueeleza suala lililotokea ambapo wazazi wa binti walitolewa nje ya kikao na baadae wazazi wa mtuhumiwa wakaambiwa wamtoroshe mwanae kwasababu kesi hiyo ni mbaya.

Aidha, Bwana Yassin Yuta (32) ametishiwa na viongozi hao na kumzuia asiendelee kufuatilia mambo ya kijiji hicho, baada ya kuonekana mnamo Aprili 17 mwaka huu akiwa na waandishi wa habari baada ya kumshutumu kutoa siri za kijiji hicho kwa vyombo vya habari na kishi kumuoanya kucha mara moja vinginevyo wanamuua.

Kufuatia sakata hilo ukaitishwa mkutano wa hadhara, siku hiyo hiyo na kusimamiwa na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bwana Mponzi na kutoa agizo kuwa Bwna Yassin asionekane katika kijiji hicho na kuwamuru wananchi wakimuona wachukue sheria mkononi au kuuawa.

Hata hivyo agizo hilo liliwashangaza baadhi ya wananchi wapenda amani kutokana na kiongozi aliyepewa dhamana kuchochochea uhalifu.

Kwa upande wake Bwana Yassin amesema ametishiwa kuuawa na Bwana Mohammed Mwangoka, Shungu Ringston(mtuhumiwa) na Ibrahim Mponzi(Mwenyekiti), ambapo ametoa taarifa katika Kituo cha Polisi Uyole na Jeshi la Polisi linafanya uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger