Pages


Home » » HAKIMU AVUNJIWA NYUMBA NA KUIBIWA - MKOANI MBEYA

HAKIMU AVUNJIWA NYUMBA NA KUIBIWA - MKOANI MBEYA

Kamanga na Matukio | 04:59 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mtu au watu wasiofahamika wamevunja na kuiba vitu kadhaa nyumbani kwa Hakimu wa Mahakama ya mwanzo Mbeya Vijijini Sadiki Mbilu.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya Barakiel Masaki, amesema wezi hao walivunja kitasa cha mlango wa nyumba ya hakimu huyo Aprili 23 mwaka huu majira ya 12:30 eneo la Sabasaba Jijini Mbeya.

Baadhi ya vitu vilivyoibiwa ni pamoja na TV flat screen inchi 32, Radio na deki yake aina ya Toshiba, DVD deki aina ya LG na King’amuzi cha Startimes vyote vikiwa na thamani ya shilingi 2,570,000/=.

Hata hivyo Kaimu Kamanda Masakai amemeongeza kuwa upelelezi wa tukio hilo unaendelea ili kubaini watu waliohusika na wizi.

Wimbi la wizi Mkoani Mbeya limeendelea kukua kwa kasi kubwa siku hadi siku ambapo baadhi ya wezi wamekuwa wakikamatwa na kupigwa na wengine kukuawa hata kwa kuchomwa moto.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger