Pages


Home » » MWENYEKITI WA MTAA AJIUZULU NA KUHAMIA CHADEMA

MWENYEKITI WA MTAA AJIUZULU NA KUHAMIA CHADEMA

Kamanga na Matukio | 05:24 | 0 comments

 Picha ya kwanza Mwenyekiti wa mtaa wa Ilolo Kati Ngambi Ngambi (Kushoto), akifuatiwa na Samson Kibole (katikati) wakiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Mbeya Bwana John Mwambigija na aliyekuwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Ilemi Joseph James Mbela, walipokuwa wakipokelewa rasmi kutokea Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuachia nyadhifa zao katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Mtaa wa Ilolo Kati. Picha ya Pili Diwani wa Kata ya Mwakibete (CHADEMA) Bwana Lucas Mwampiki akionesha kadi zilizopokelewa kwa wanachama wa CCM ambao wamejiunga na CHADEMA.
Picha ya Tatu  Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Mbeya Bwana John Mwambigija na akimtambulisha rasmi aliyekuwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Ilemi Joseph James Mbela, mara baada ya kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Picha ya Nne Ngambi K Ngambi akionesha rasmi kadi ya CCM na kumkabidhi Diwani wa Kata ya Sinde mheshimiwa Fanuel Kyanula (CHADEMA) mwenye shati ya rangi nyeusi.
*******
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Wimbi la Wenyeviti wa Mitaa kujuzulu kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), na kuhamia CHADEMA limeingia katika sura mpya, baada ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Ilolo Kati Bwana Ngambi K Ngambi naye kujiuzulu.

Tukio hilo limetokea Aprili 24 mwaka huu katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika mtaa huo na kuhudhuriwa na baadhi ya madiwani wa CHADEMA jijini Mbeya wakiwemo madiwani wa Kata za Mwakibete, Forest, Sinde ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Mkutano huo.

Akifungua mkutano huo Diwani wa Kata ya Sinde Mheshimiwa Fanuel Kyanula, alitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Sinde ambapo kila mwananchi alikuwa akichangia shilingi 3,000 badala ya shilingi 10,000 za awali.

Aidha mchango huo umesaidia kumalizia kabisa ujenzi wa madarasa hayo, amewashukuru wananchi kwa kuitikia wito wa kuchangia mchango huo bila usumbufu na kipingamizi cochote.

Diwani Kyanula akielezea matumizi ya mchango huo umeweza kukidhi kazi ya upigaji wa sakafu na uwekaji wa nyaya za umeme, hatua hiyo ambayo Mkurugenzi wa Halmashauri alitoa pongezi kwa na usimamizi mzuri hadi kufikia kukamilika kwa ujenzi huo.

Naye Diwani wa Kata ya Mwakibete Bwana Lucas Mwampiki amempongeza mwenyekiti huyo wa mtaa Bwana Ngambi na kwamba ni kiongozi mchapa kazi, hodari na hivyo wao kwa sasa wamempata Kamanda ambaye ataongoza mapambano dhidi ya ubadhilifu.

Kwa upande wake Bwana Gambi amesema kujiunga kwake CHADEMA ni hiari yake na wala hajalazimishwa na mtu bali ni kuchoshwa ba ukandamizaji ambavyo vilikuwa vikifanywa na CCM naye kwa kuwaonea huruma wananchi aliokuwa akiwaongoza.

Katika mkutano huo watu kadhaa walikabidha Kadi za CCM wakiwemo Rose Mwashilindi (50), Atusekelege Asumbisye (52), ambaye alikuwa balozi wa mtaa huo na Samson Mwakibole.

Katika hadhara hiyo Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Mbeya Bwana John Mwambigijaaliwapongeza waliohamia kwa hiari yao kujiunga na Chama hicho na kudai kina watu makini ndio maana kimekua kikipata mafanikio siku hadi siku na kutamba 2015 wataichukua dola.

Kuhama kwa Ngwambi aliyekuwa Mwenyekiti wa mtaa wa Ilemi ni pigo kubwa kwa CCM kwa kipindi cha hivi karibuni kwani Mwenyekiti wa mtaa wa Ilemi Bwana James Joseph Mbela naye alihamia CHADEMA akidia amechoshwa na ufisadi uliokithiri ndani ya CCM.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger