Pages


Home » » WAZIRI MAGHEMBE - SIWEZI KUPINGA UAMUZI WA VIONGOZI WA MKOA KUZUIA UUNZWAJI WA KAHAWA MBIVU.

WAZIRI MAGHEMBE - SIWEZI KUPINGA UAMUZI WA VIONGOZI WA MKOA KUZUIA UUNZWAJI WA KAHAWA MBIVU.

Kamanga na Matukio | 06:55 | 0 comments
Waziri wa Chakula, Kilimo na Ushirika Profesa Jumanne Maghembe.
******
Habari na Mwandishi wetu.
Waziri wa kilimo chakula na Ushirika Profesa Jumanne Maghembe amesema kuwa hawezi kupinga maamuzi ya viongozi wa wilaya za Mbeya, Ileje, Rungwe na Mbozi kuhusu uamuzi wa kupinga biashara ya uuzaji wa Kahawa Mbivu. 

Amesema kuwa hawezikutengua kanuni za Wizara na Bodi ya kahawa juu ya ununuzi wa kahawa mbivu na kuitaka Serikali mkoani Mbeya kusimamia sheria na kuhakikisha bei kwa wakulima wa kahawa zinakuwa nzuri ili wakulima waweze kunufaika kupitia kilimo chao.

Naye mkurugenzi wa bodi ya kahawa nchini Adolph Kumbulu na mwanasheria wa Wizara ya kilimo amesema kuwa ununuzi wa kahawa mbivu umeongeza tija ya ubora wa kahawa Tanzania kutokana na ubora wa usindikaji wake tofauti na usindikaji unaofanywa na wakulima.

Kwa upande wao viongozi wa mkoa wa Mbeya walisimama katika masimamo wao wa kutoruhusu uuzaji wa kahawa Mbivu kwani umelenga kuwanyonya wakulima wadogo wadogo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger