Pages


Home » » MGOMO WA MADAKTARI HOSPITALI YA RUFAA, MBEYA NINI TAMATI YAKE?

MGOMO WA MADAKTARI HOSPITALI YA RUFAA, MBEYA NINI TAMATI YAKE?

Kamanga na Matukio | 04:26 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya
Mgomo wa madakta Hospitali ya Rufaa, Mbeya umeendelea huku madaktari hao wakidai kuwa mgomo huo utakuwa endelevu hadi hapo Serikali itakapo tekeleza madai yao.

Katika mgomo huo madaktari hao wamesema mgomo wao umelenga kuishinikiza Serikali kuboresha huduma za afya, kuowaongezea mshahara, posho na malipo ya kazi hatarishi pamoja na kuwapatia makazi kama ambavyo sheria ya nchi inavyoelekeza.

Akiongea na waandishi wa habari mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Mbeya Dokta Eliuta Sanker amesema mgomo huo umefanywa na madaktari wanafunzi 65 na madaktari wapya 10.

Mgomo huo wa madaktari ulianza January 23 mwaka huu baada ya mwenyekiti wa kamati ya muda wa jumuiya madaktari hao Stephano Ulimboka kutangaza mgomo usio na kikomo hadi madai yao yatakapotekelezwa
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger