Pages


Home » » WANAWAKE WA KANISA LA MORAVIAN JIMBO LA KUSINI MAGHARIBI WAPEWA MSAADA WA MAJIKO NA TAA AMBAZO HUTUMIA MIOZI YA JUA

WANAWAKE WA KANISA LA MORAVIAN JIMBO LA KUSINI MAGHARIBI WAPEWA MSAADA WA MAJIKO NA TAA AMBAZO HUTUMIA MIOZI YA JUA

Kamanga na Matukio | 05:33 | 0 comments
 Idara ya Wanawake na watoto Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Magharibi Tanzania limepokea misaada mbalimbali ikiwemo ya taa na jiko ambavyo vinazotumia miozi ya jua, ambapo msaada huo umetolewa na Kanisa la Moravian Ujerumani kwa ajili ya kuiwezesha idara hiyo kujikomboa kiuchumi.
 Jiko linalotumia miozi ya jua lenye thamani ya shilingi laki 5, lililotolewa na Kanisa la Moravian Ujerumani kwa ajili ya kuiwezesha Idara ya Wanawake na watoto kwa lengo kujikomboa kiuchumi, ambapo Jimbo hilo limepokea msaada wa majiko matatu na taa ishirini na tano, ambapo taa hiyo inakodishwa kwa shilingi elfu nne kwa mwezi..
Pichani ni Bi Ester Jonas Mwanzembe, akionesha bidhaa mbalimbali ambazo huzalishwa na wanawake wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Magharibi, ikiwa ni pamoja na virutubisho vya chakula na divai. 

Hitmisho:- Kanisa hilo limemteua mchungaji Lawrence Nzowa kwenda nchi ya Ethiopia kwa muda wa miezi miwili kwa lengo la kusomea taaluma ya utengenezaji wa taa na jiko ambapo vyote vinatumia miozi ya jua.

Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger