Pages


Home » » RAIA 27 WA SOMALIA WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI KINYUME NA SHERIA - MBEYA

RAIA 27 WA SOMALIA WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI KINYUME NA SHERIA - MBEYA

Kamanga na Matukio | 05:41 | 0 comments
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi.
***** 
Habari na Mwandishi wetu.
Raia 27 wa Somalia wanashikiliwa na Jeshi la polisi mkoa wa Mbeya kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha Sheria.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amesema kuwa raia hao wa kigeni wamekamatwa jana maeneo ya Nonde jijini hapa wakati polisi wakiwa katika doria.

Amesema kati ya raia hao mmoja ndiye aliyeweza kujitambulisha kwa jina Genesis Basema mwenye umri wa miaka 26 na kuongeza kuwa raia hao walikuwa wakiishi kwenye pagara kwa muda usiojulikana.

Wakati huohuo Kamanda Nyombi ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa kwa Jeshi la polisi pindi wanapokuwa na taarifa ya kuwepo kwa raia wowote wa kigeni hapa nchini ili kudhibiti vitendo vya uvamizi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger