Pages


Home » » WATU WAWILI WAZIKWA HAI MKOANI MBEYA KWA TUHUMA ZA MAUAJI KWA IMANI ZA KISHIRIKINA.

WATU WAWILI WAZIKWA HAI MKOANI MBEYA KWA TUHUMA ZA MAUAJI KWA IMANI ZA KISHIRIKINA.

Kamanga na Matukio | 02:53 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Sakata la Kifo cha Mzee Nongwa Hussein Mkazi wa Kijiji cha Kalungu, Kata ya Ivuna, Tarafa ya Kamsamba, Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya, kilichotokea Januari 13 mwaka huu majira ya saa 10 jioni hali iliyopelekea vijana wenye hasira kali kuhusisha kifo hicho na imani za kishirikina na kupelekea watu wawili kati ya watatu kuzikwa hai.

Walioshutumiwa na kuhusika na kifo hicho kwa imani za kishirikina ni pamoja na kaka wa marehemu Bwana George Hussein, Ernest Molela na Bi. Miziana  Nachela wote wakazi wa kijiji hicho.

Wakati mazishi yakiendelea baada ya kuchonga jeneza la marehemu vijana hao walianza kumtafuta kaka wa marehemu huyo ambaye alifanikiwa kutoroka kusikojulikana, na baadae kufanikiwa kuwakamata Bwana Molela na Bi. Nachela na kisha kuanza kuwaporomoshea kipigo  na kuwazika hai katika kabuli moja na marehemu Nongwa na hivyo kuzikwa watu watatu katika kaburi moja.

Baada ya sakata hilo vijana hao waliondoka makaburini na taarifa kumfikia Afisa Mtendaji wa Kata hiyo Bwana Joseph Silwimba Mengwa, ambaye alifika eneo la tukio na kukuta kitendo hicho cha kikatili kimekwisha tendeka na yeye kuchukua jukumu la kulitaarifu Jeshi la Polisi ambao siku ya pili Januari 14 mwaka huu majira ya saa tatu asubuhi lilifika eneo la tukio na kuifukua miili hiyo ya watu waliozikwa hai.

Aidha, miili hiyo ilikabidhiwa kwa wanandugu ili kuzikwa upya katika makaburi mengine huku wakiuacha mwili wa marehemu Nongwa katika kabuli la awali.

Uchunguzi wa awali umeonesha kuwa baadhi ya vijana waliohusika na tukio hilo wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na wakati wowote mara baada ya upelelezi kukamilika watafikishwa mahakamani.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoani hamo Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na amewataka wananchi kutojichukulia sheria mikononi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger