Pages


Home » » Chama cha wachezaji wa kulipwa nchini Uingereza PFA, kimemkana winga kutoka nchini ubelgiji na klabu ya Chelsea Eden Hazard.

Chama cha wachezaji wa kulipwa nchini Uingereza PFA, kimemkana winga kutoka nchini ubelgiji na klabu ya Chelsea Eden Hazard.

Kamanga na Matukio | 02:12 | 0 comments
Eden project: How Hazard will look in Chelsea blue 
 Eden Hazard
  Na Shaban Kondo.
 Chama cha wachezaji wa kulipwa nchini Uingereza PFA, kimemkana winga kutoka nchini ubelgiji na klabu ya Chelsea Eden Hazard kufuatia sakata la kumpiga kijana anaeokota mipira katika uwanja wa Liberty Charlie Morgan wakati wa mchezo wa pili wa hatua ya nusu fainali ya kombe la ligi uliochezwa usiku wa kuamkia jana.

Chama cha wachezaji wa kulipwa nchini Uingereza PFA, kimemkana winga huyo kupitia kwa mtendaji wake mkuu Gordon Taylor ambapo amesema Eden Hazard hana mamlaka ya kujichukulia sheria mkononi, zaidi ya kuacha sheria zilizotungwa zichukue mkondo wake juu ya sakata la kumpiga kijana muokota mipira. 

Amesema tukio hilo moja kwa moja linajidhihirisha wazi kwamba chama cha soka nchini Uingereza kitamuadhibu mchezaji huyo kutokana na kile alichokitenda na wao kama chama cha wachezaji wa kulipwa hawawezi kuingilia kutokana na hali halisi kutohitaji utetezi.

Hata hivyo Gordon Taylor amesema bado wanasubiri taarifa rasmi kutoka FA kama itawafikia na endapo watahitajika kwa ajili ya kumtetea mchezaji huyo watajitokeza lakini wanaamini kisu cha sheria kitamkata Eden Hazard.

Katika hatua nyingine meneja wa klabu ya Chelsea Rafael Benitez amekiri mchezaji wake alifanya makosa makubwa ya kumpiga kijana huyo, lakini bado akaendelea kusisitiza kwamba bado suala hilo lina wigo mpana wa kujadiliwa.

Hata hivyo Benitez ameshauri suala hilo kutazamwa upya kutokana na kijana Charlie Morgan kuchangia kitendo alichofanyiwa kufuatia kitendo cha kuupiga mpira kabla ya kutaka kuukota, na hivyo kumsababishia Hazard kuamini huenda alikua anapoteza muda kwa makusudi.

Wakati huo huo Eden Hazard ameomba radhi kufautia kitendo cha kumpiga Charlie Morgan kwa kusema halikua kusudio lake kumpiga kijana huyo bali alitaka kuupiga mpira na kwa bahati mbaya alijikuta anafanya tofauti.

Amesema anajua jamii itayapokea maneno hayo tofauti lakini amesisitiza ukweli ndio huo na hana lingine la kusema zaidi ya kumtaka radhi Charlie Morgan pamoja na jamii ya soka ulimwenguni kote.

Baada ya kitendo hicho Eden Hazard alionyeshwa kadi nyekundu huku akiiacha timu yake ikiangamia kwa kutolewa kwenye michuano ya kombe la ligi dhidi ya Swansea ambao wametinga katika hatua ya fainali kwa jumla ya mabao mawili kwa sifuri waliyoyapata katika mchezo wa awali kabla ya usiku wa kuamkia jana ambapo waliambulia matokeo ya sare ya bila kufungana.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger