Pages


Home » » Mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatusi Kinawiro amewataka wakulima kugharamia pembejeo za kilimo

Mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatusi Kinawiro amewataka wakulima kugharamia pembejeo za kilimo

Kamanga na Matukio | 02:15 | 0 comments
Mkuu wa wilaya ya Chunya Ndugu Deodatus Kinawiro.

Chanzo;- Bomba FM Mbeya.

Mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatusi Kinawiro amewataka wakulima kugharamia pembejeo za kilimo ambazo zipo tayari kwa mawaka badala ya kusubiria vocha za Ruzuku.



Ameyasema hayo kufuatia kuwepo kwa malalamiko ya wananchi wilayani Chunya kuhusu kucheleweshewa vocha za Ruzuku na kwamba mbolea na mbegu zimepelekwa karibu na wananchi kwa hiyo wakulima wanapaswa kwenda kununua kwa mawakala, ila ruzuku ni bado tatizo nila mbegu zimeletwa OPV badala ya Chotara.

Amesema sehemu kubwa ya wananchi wanamiliki mashamba yenye ukumbwa wa zaidi ya heka moja huku ruzuku ya Serikali inatolewa kwa mkulima aliye na shamba lenye ukubwa wa heka moja kwani hutolewa mbegu mbolea ya kupandia na kukuzia.

Aidha, ameelezea changamoto kubwa ni kuwa ruzuku hizo zinapotolewa lakini huwa ni tofauti kwani wananchi hawazitumii na badala yake wanaziuza na wanapaswa kuwa wawazi kwa sababu serikali ilishawajengea kwa miaka tangu ya 2008/2009 na wananchi waliofaidika ni zaidi ya 30000.

Kuhusu maafa yatokanayo na mvua Mkuu huyo wa wilaya Deodatus Kinawiro amesema maafa yaliyotokea si makubwa ukilinganisha na mwaka jana, licha ya Kata ya Mbugani nyumba kama 18 ziliezuliwa kutokana na mvua na upepo lakini anashukuru wananchi wameweza kuezeka nyumba hizo kwa bati na wengine wamejiwekeza kwa ndugu zao lakini suala la barabara linapotokea tatizo sehemu korofi huzirekebisha na magari kuendelea kupita.
 
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger