Pages


Home » » Chama cha wakulima AFP Leo kimekutana na tume ya kukusanya maoni ya katiba mpya .

Chama cha wakulima AFP Leo kimekutana na tume ya kukusanya maoni ya katiba mpya .

Kamanga na Matukio | 04:04 | 0 comments
Chama cha wakulima AFP Leo kimekutana na tume ya kukusanya maoni ya katiba mpya na kutoa mapendekezo yao wakitaka katiba mpya ijayo itaje idadi ya wizara zisizozidi 15 ikiwemo wizara mpya itakayoshughulika na mafuta pekee.



Katibu Mkuu AFP Rashid Rai amesema mafuta kuwekwa wizara moja na madini siyo sawa kwa kuwa watendaji Wanakuwa na tamaa zaidi ya kushughulikia madini kwa sababu ya maslahi yao binafsi na si kwa maslahi ya Taifa kujikwamua kiuchumi.



Akizungumzia suala la kuwa na Serikali moja naibu Mkurugenzi wa uenezi na habari wa chama hicho Shaban Akwitimba amesema katiba itoe fursa kwa kiongozi kuondolewa madarakani.



Mwenyekiti wa chama cha NLD Dokta Emmanuel Makaidi amependekeza katiba mpya ijayo iwape haki wananchi ya kuwa na uwezo wa kumkataa mbunge wa kuchaguliwa kutokana na udhaifu katika utendaji kazi.



Utoaji wa maoni kwa vyama vya siasa umeanza jana kwa CCM, CHADEMA na CUF na hii leo ni zamu ya chama cha wakulima AFP, NLD na DP na kufanya idadi ya vyama vilivyotoa maoni yao kwa tume ya katiba mpya kufikia sita.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger