Pages


Home » » Vuguvugu la kurudisha Fomu za kuwania Uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania TFF na bodi ya Ligu Kuu Tanzania TPL Board.

Vuguvugu la kurudisha Fomu za kuwania Uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania TFF na bodi ya Ligu Kuu Tanzania TPL Board.

Kamanga na Matukio | 03:46 | 0 comments
Kwa hisani ya Shaban Kondo.
Wakati leo ndiyo mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi za uongozi wa shirikisho la soka nchini TFF pamoja na bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) mpaka jana waliochukua fomu 36 huku wadau 18 wakizirejesha.

Afisa habari wa shirikisho la soka nchini TFF Boniface Wambura amesema idadi hiyo ni kufikia leo mchana lakini akasisitiza matarajio ya idadi ya wadau waliochukua fomu kuongezeka itakapofika leo alasiri ambapo ndio itakua mwisho wa kurejesha fomu kwa muyjibu wa utaratibu uliotangazwa na kamati ya uchaguzi.

Wakati mchakato wa uchaguzi wa TFF ukiendelea hivyo, aliekuwa katibu mkuu wa FAT kwa sasa TFF Michael Richard Wambura amekua miongoni mwa wadau waliojitokeza kurejesha fomu za kuwani nafasi ya umakamu wa raisi.

Wambura amerejesha fomu hizo, huku akiwahusia waandishi wa habari jambo la kuwa waadilifu katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi wa TFF uliopangwa kufanyika February 24 jijini Dar es salaam.

Wakati huo huo aliekua muamuzi mahiri Omari Abdul Kadir nae amejitosa kuchukua fomu za kuwania nafasi ya ujumbe wa kamati ya Utendaji Kanda ya Dar es salaam.

Omari Abdul Kadir amesema kilichomzuta hadi kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo ni kutaka kurekebisha masuala kadha wa kadha ndani ya TFF lakini kubwa ni suala la waamuzi ambao imefikia wakati wanaangushiwa vipondo wanapokua katika majukumu yao.


Orodha kamili ya waombaji ni Athuman Nyamlani, Jamal Malinzi na Omari Mussa Nkwarulo (urais) wakati waombaji wa umakamu wa rais mpaka sasa ni Michael Wambura, Ramadhan Nassib na Wallace Karia.

Kwa upande wa wajumbe wa Kamati ya Utendaji na kanda zao kwenye mabano ni Salum Chama (Kagera na Geita), Mugisha Galibona, Samuel Nyalla, Titus Osoro na Vedastus Lufano (Mara na Mwanza).

Epaphra Swai na Mbasha Matutu (Shinyanga na Simiyu), Charles Mugondo na Elly Mbise (Arusha na Manyara), Yusuph Kitumbo (Kigoma na Tabora), Ayubu Nyaulingo, Blassy Kiondo, Nazarius Kilungeja na Selemani Kameya (Katavi na Rukwa) na James Mhagama (Njombe na Ruvuma).

Athuman Kambi na Zafarani Damoder (Lindi na Mtwara), Hussein Mwamba na Stewart Masima (Dodoma na Singida), Farid Nahdi, Geofrey Nyange na Twahili Njoki (Morogoro na Pwani), Elias Mwanjala na Eliud Mvella (Iringa na Mbeya), Khalid Mohamed (Kilimanjaro na Tanga) na Muhsin Balhabou, Omari Abdulkadir na Shaffih Dauda (Dar es Salaam).

Kwa upande wa Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board) waliochukua fomu mpaka sasa ni wawili tu. Yusuf Manji amechukua fomu ya uenyekiti wakati Said Mohamed amechukua fomu ya kuwania umakamu mwenyekiti.

Shirikisho la soka nchini TFF limeendelea kusisistiza tarehe ya kuanza kwa mzunguuko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania bara kwa kuviarifu vilabu vinavyoshiriki ligi hiyo.

Afisa habari wa TFF Boniface Wambura amesema mzunguuko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania bara utaanza Januari 26 kama ulivyokua umepangwa lakini kuna baadhi ya michezo itafanyiwa marekebisho kufuatia maombi ya televisheni ya SuperSport ya kutaka kuonyesha michezo ya Super Week kama ilivyokuwa katika mzunguko wa kwanza.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger