Pages


Home » » Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji, imeliondoa shauri lililokuwa mbele yake dhidi ya klabu ya Simba lililowasilishwa na wachezaji Pascal Ochieng na Daniel Akuffo baada ya pande hizo kufikia makubaliano.

Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji, imeliondoa shauri lililokuwa mbele yake dhidi ya klabu ya Simba lililowasilishwa na wachezaji Pascal Ochieng na Daniel Akuffo baada ya pande hizo kufikia makubaliano.

Kamanga na Matukio | 02:32 | 0 comments

Na Shaban Kondo.
Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji iliyokutana Januari 19 mwaka huu chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa imeliondoa shauri lililokuwa mbele yake dhidi ya klabu ya Simba lililowasilishwa na wachezaji Pascal Ochieng na Daniel Akuffo baada ya pande hizo kufikia makubaliano.

Afisa habari wa shirikisho la soka nchini TFF Bonifas Wambura amesema wachezaji hao kutoka nchini Kenya na Ghana waliwasilisha malalamiko mbele ya kamati wakipinga kukatizwa kwa mikataba yao bila kulipwa haki stahili.

Kama itakumbukwa vyema Pascal Ochieng anaecheza nafasi ya ulinzi alitangaza msimamo wake mwishoni mwa mwaka jana kupitia kipindi hiki kwa kudai atahakikisha analipwa haki zake stahiki, baada ya uongozi wa Simba kumuondoa kwenye orodha ya wachezaji waliosajiliwa na klabu hiyo katika kipindi cha dirisha dogo la usajili.

Ochieng alitangaza msimamo huo, baada ya kluwasilisha vielelezo vyake katika ofisi za shirikisho la soka nchini TFF ambavyo vilikua vinainisha makubaliano yaliyokuwepo kati yake na uongozi wa klabu ya simba uliomsajili mwanzoni mwa msimu huu akitokea Johor FC ya nchini kwao Kenya.

Wakati huohuo Msanii wa kizazi kipya Hussein Rashid * Hussein Machozi* ameonyeshwa kushangazwa na uteuzi wa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Sylvester Mash kwa kudai kocha huyo hana sifa za kutosha katika wadhifa waliopewa.

Hussein Rashid amesema kushangazwa na uteuzi wa kocha huyo alipohojiwa na kipindi hiki ambapo amaaleza kwamba Sylvester Mash ni kocha ambae hakupendezwa nae wakati akicheza soka akiwa na klabu ya Kagera Sugar, baada ya kuona alidhamiria kukiua kipaji chake ambacho kilikua chanzo cha kusajiliwa na klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya soka Tanzania bara.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger