Pages


Home » » Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dakta Norman Sigala ameitaka jamii kuendelea kuchangia shughuli za kimaendeleo katika elimu.

Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dakta Norman Sigala ameitaka jamii kuendelea kuchangia shughuli za kimaendeleo katika elimu.

Kamanga na Matukio | 02:54 | 0 comments
  Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dk.Norman Sigalla akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.


Habari kamili na Gabriel Mbwille.
Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dakta Norman Sigala ameitaka jamii kuendelea kuchangia shughuli za kimaendeleo katika elimu ili kuwawezesha wanafunzi kuanza elimu ya Sekondari kwa wakati.



Ameyasema hayo leo katika mkutano wa hadhara wenye lengo la kuhamasisha maendeleo ya elimu katika halmashauri ya wilaya ya Mbeya vijijini amesema wazazi wanapaswa kuchangia maendeleo, na walimu wakishatengenezewa mazingira mazuri ya kufundisha hakuna mwali ambaye anakuwa mvivu.



Aidha amewataka wanafunzi wa shule ya Sekondari Usongwe kuwa na nidhamu masomoni ili waweze kufikia malengo waliyoyakusudia na kufikia Januari 30 mwaka huu vyumba vya madarasa katika shule hiyo vitakuwa vimekamilika ili kutoa furasa kwa wanafunzi kusoma kwa uhuru.



Dakta Sigala ametoa pongezi kwa wananchi waliowekeza katika kuchangia maendeleo ya elimu na amewaagiza wananchi hao kuwafahamisha wananchi wenzao kuwa hakuna elimu bora inayopatikana bila kuchangia kwa hiyo hawana budi kukata tama ya kutoa michango pindi wanapohitajika kuchangia.



Kwa upande wao waalimu wa shule hiyo wameiomba Serikali kuangalia namna ya kupunguza makato kwa waalimu ili kuwawezesha kuwa na kipato kikubwa kitakachowawezesha kujikimu kimaisha.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger