Pages


Home » » Hakimu na Afisa Mtendaji wa Kata matatani kwa tuhuma za Rushwa wakamatwa na TAKUKURU.

Hakimu na Afisa Mtendaji wa Kata matatani kwa tuhuma za Rushwa wakamatwa na TAKUKURU.

Kamanga na Matukio | 03:48 | 0 comments
Chanzo Bomba FM Mbeya 104,0MHz 
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Mbeya imewakamata na kuwafikisha mahakama ya Wilaya ya Rungwe, hakimu wa mahakama ya mwanzo ya Kata ya Lupata Andrew Siwale na afisa mtendaji wa kata ya Kisegese Gasper Bagomoke kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa pamoja na vitendo vya uonevu hasa kwa watu wasio na kipato.


Wakiongea na Bomba FM wananchi wa eneo husika wamesema watendaji wa kata hiyo wamekuwa wakimtoza faini mwananchi hadi shilingi laki tatu kwa kosa moja na kuteswa kwa mwananchi asiyekuwa na kipato cha kutosha cha kulipia faini.


Kwa upande wake afisa mtendaji wa kata hiyo Bwana Bagomoke amekiri kuwa hakimu huyo kuchukuwa fedha kwa watuhumiwa wanaobainika na makosa mbalimbali na kuwaagiza Migambo kuwanyanyasa wananchi pamoja kuwatoza faini kwa kuwapandikizia kesi.


Aidha, akiongelea sakata hilo Mkuu wa Taasisi ya hiyo mkoani hapa Daniel Mtuka amesema viongozi hao wamekamatwa January 15 katika maeneo mawili tofauti mmoja akiwa Kata ya Kisegese na mwingine kata ya Itete na kasha kuhojiana nao na kupata ushahidi.


Amesema viongozi hao waliunda mahakama yao kinyume cha kanuni za Serikali ambapo kesi zao zilikuwa zikiendeshwa nyakati za jioni na usiku na kesi kuanzia saa 12 kusikilizwa kukiwa hakuna karatasi zozote zinazohusikana na mahakama, bendera, picha za viongozi na risiti za faini na wakati mwingine kama jingo likiwa na tatizo la umeme ukikatika vibatali vilikuwa vikiwashwa ili kesi iweze kumalizika.


Mtauka amesema watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani kwa kifungu namba 15 kifungu kidogo cha kwanza na cha pili cha mwaka 2007, cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa cha kuomba na kupokea rushwa, ambapo mlalamikaji aliomba rushwa ya shilingi laki mbili kufuatia kesi ya awali ya msingi ya kwa wizi na kuharibu mali kati ya Bi Elizabeth Mlenga na mlalamikaji.


Wakati huohuo TAKUKURU imejipanga kikamilifu katika kukomesha vitendo vya uonevu vinavyofanywa na watendaji wa Serikali katika mahakama ya mwanzo na mabaraza ya kata ili haki ya msingi kupatikana kwa maslahi ya wananchi na viongozi.


Hata hivyo kuhusu faini anayotakiwa kutozwa mwananchi katika mabaraza ya kata Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abasi Kandoro amewataka viongozi wa mabaraza hayo kutomtoza mwananchi kiasi kikichozidi shilingi elfu kumi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger