Pages


Home » » TBL yakabidhi vifaa vya Michezo kwa Klabu kongwe nchini Simba na Yanga,

TBL yakabidhi vifaa vya Michezo kwa Klabu kongwe nchini Simba na Yanga,

Kamanga na Matukio | 02:10 | 0 comments
Na Shaban Kondo,
 Wadhamini wa klabu kongwe nchini Simba na Yanga, kampuni ya bia nchini TBL kupitia bia yake ya Kilimanjaro jana wamekabidhi vifaa vya michezo kwa viongozi wa klabu hizo kwa ajili ya mzunguuko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania bara.

Akikabidhi vifaa hivyo meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe amesema wanaamini klabu hizo kongwe zimejiandaa vyema na zipo tayari kwa mshike mshike wa ligi mzunguuko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania bara unaoatarajiwa kuanza siku ya jumamosi.

Baada ya kupokea vifaa hivyo katibu mkuu wa klabu ay Dar es salaam young Africans Lawrence mwalusako amesema wamefarijika kupata vifaa hivyo ambapo hatua hiyo bado inaendelea kutamani kufanya kazi na kampuni ya bia nchini TBL kufuatia utaratibu wake wa kufanya kazi kwa kufuata mkataba unavyoelekea.

Kwa upande wa mabingwa wa soka Tanzania bara Wekundu wa Msimbazi Simba ambao waliwakilishwa na msemaji wao Ezekiel Kamwaga katika hafla hiyo wameishukuru kampuni ya bia nchini TBL na wameahidi kufanya jitihada za kutetea ubingwa wao msimu hukua kikumbushia mazuri ambayo wamekua wakiyafanya katika miaka inayoishia na tatu.

Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger