Pages


Home » » RAIS AKERWA NA UTENDAJI MBOVU WA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA NZEGA.

RAIS AKERWA NA UTENDAJI MBOVU WA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA NZEGA.

Kamanga na Matukio | 04:02 | 0 comments
 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa maelekezo kwa Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli, Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe na Waziri wa Fedha Dkt William Mgimwa kabla hajahutubia Jumatatu mkutano mkubwa wa hadhara mjini Nzega katika ziara yake ya siku nne ya mkoa wa Tabora ambapo anazindua miradi kadhaa ya maendeleo ikiwemo barabara, daraja na maji.

(PICHA NA IKULU)

 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisikiliza maelezo ya Meneja wa TANESCO wa Nzega akielezea mikakati ya kuwapatia wakazi wa hapo nishati hiyo Jumatatu mkutano mkubwa wa hadhara mjini Nzega katika ziara yake ya siku nne ya mkoa wa Tabora ambapo anazindua miradi kadhaa ya maendeleo ikiwemo barabara, daraja na maji.

 

Umati wa wananchi ukiwa katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Rais Jakaya Kikwete mkoani Tabora leo

 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea ripoti ya maendeleo ya Wilaya ya Uyui toka kwa mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Lucy Mayenga wakati Rais alipowasili Tabora mjini kuendelea na ziara yake ya  siku nne ya mkoa wa huo ambapo anazindua miradi kadhaa ya maendeleo ikiwemo barabara, daraja na maji. 

Habari Kamili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete amekerwa na utendaji kazi mbovu wa mkurugenzi wa halmashari ya Nzega mkoani Tabora, baada ya mkurugenzi huyo kushindwa kuwapatia wananchi wake huduma ya maji safi.



Awali akiongea kwenye mkutano huo wa hadhara mbunge wa jimbo la Nzega Hamisi Kigangwala amesema pamoja na vikao vya halmashauri kutoa kipaumbele katika mradi wa maji bado mkurugenzi huyo amekuwa akiukataa.



Naye waziri wa maji Profesa Jumanne Maghembe amesema kitendo cha halmashauri hiyo kukosa maji ni cha aibu ambapo amesema kwa nafasi aliyonayo mhandisi wa maji wilayani humo lazima awajibishwe.



Akiongea huku akionekana mtu aliyesikitishwa kusikia wananchi wake wakikosa maji safi na salama licha ya kuwepo kwa mipango mingi ya kuboresha huduma hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Kikwete amesema hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mkurugenzi huku akiwaahidi wananchi hao huduma ya maji safi na salama.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger