Pages


Home » » Wadhamini wa ligi kuu ya soka Tanzani bara wametangaza kuwa tayari kwa kipyenga cha mzunguko wa pili wa ligi hiyo'

Wadhamini wa ligi kuu ya soka Tanzani bara wametangaza kuwa tayari kwa kipyenga cha mzunguko wa pili wa ligi hiyo'

Kamanga na Matukio | 02:10 | 0 comments
Na Shaban Kondo. Wadhamini wa ligi kuu ya soka Tanzani bara wametangaza kuwa tayari kwa kipyenga cha mzunguko wa pili wa ligi hiyo kitakachopulizwa kuanzia Januari 26 mwaka huu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam, Meneja Mahusiano ya Nje wa Kampuni ya Vodacom inayodhamini ligi kuu, Salum Mwalim amesema kwamba kampuni yake inajisikia fahari kuona soka sasa inachezwa viwanjani zaidi na si nje hivyo wanatarajia upinzani mkubwa katika mzunguuko wa pili.

Salum Mwalim pia akatoa shukurani kwa TFF pamoja na kwa kamati ya Ligi kufautia ushirikiano mzuri wanaowaonyesha, katika kuendeleza na kuleta chachu ya ligi kuu ya soka Tanzania bara ambayo mwanzoni mwa msimu huu ilianza kwa changamoto kadha wa kadha.

Wakati huo huo shirikisho la soka nchini TFF kupitai kwa Afisa habari Bonifas Wambura limetoa kauli ya kuwa tayari kwa kipyenga cha mzunguko wa pili, kupulizwa baada ya kukamilisha maandalizi yote yanayostahili.

Michezo ya ligi kuu itakayochezwa mwishoni mwa juma hili ni kati ya;


African Lyon
 - 
SIMBA Sports Club
Mtibwa Sugar
 - 
Police Morogoro
Coastal Union
 - 
Mgambo JKT
Ruvu Shooting
 - 
JKT Ruvu
Azam
 - 
Kagera Sugar
JKT Oljoro
 - 
Toto Africans


Wakati matayarisho ya mzunguuko wa pili wa ligi kuu msimu huu yakiwa katika mstari wa mafanikio kwa mara ya kwanza wadhamini wa ligi hiyo kwa kushirikiana na kampuni ya LAJANN E-SYSTEMS ENTERPRISE wamezindua tovuti maalum itakatohusika na ligi kuu. 

Daniel Mwakamele msemaji wa msemaji wa Kampuni ya LAJANN amesema wamefanikisha uzinduzi huo baada ya kufanya kazi kwa umakini huku wakiamini kila mtanzani watakua akipata taarifa za ligi kwa wakati na kwa umakini.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger