Pages


Home » » Kamati ya uchaguzi ya TFF imeendelea imetoa taarifa ya kurekebisha orodha ya pingamizi iliyotolewa katika vyombo vya habari.

Kamati ya uchaguzi ya TFF imeendelea imetoa taarifa ya kurekebisha orodha ya pingamizi iliyotolewa katika vyombo vya habari.

Kamanga na Matukio | 02:42 | 0 comments

Na Shaban Kondo,

Kamati ya uchaguzi ya shirikisho la soka nchini TFF imeendelea imetoa taarifa ya kurekebisha orodha ya pingamizi iliyotolewa katika vyombo vya habari kwa kueleza iliacha pingamizi lililowekwa na Paul Mhangwa dhidi ya Mugisha Galibona na Vedastus Lufano ambao wanaomba nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji ya TFF kupitia kanda ya pili (Mwanza na Mara).

Kamati ya uchaguzi ya TFF iomeomba radhi kwa pingamizi hilo kuachwa kwenye orodha iliyotolewa hapo jana katika vyombo vya habari, hivyo imesisitiza wahusika hao kufika bila kukosa katika kiksoi cha kujadili pingamizi kitakachofanyika jumatano Januari 30 katika ofisi za TFF kuanzia saa nne asubihi.

Katika hatua nyingine kamati ya uchaguzi ya TFF imewataka walioweka pingamizi dhidi ya wagombea nafasi mbali mbali za uongozi wa TFF kuwa na ustahamilivu katika kipindi hiki kwa ajili ya kuiachia kamati hiyo kufanya kazi yake ipasavyo.

Akizungumza kwa niaba ya kamati hiyo katibu mkuu wa TFF Angetille Osiah amesema hairuhusiwi kwa yoyote alioweka pingamizi dhidi ya wagombea kwenda katika vyombo vya habari na kuliweka wazi pingamizi lake.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger