Pages


Home » » Walcott atoboa siri, Tevez alifikiria kustaafu soka kufuatia ugomvi wake na Kocha Mancini.

Walcott atoboa siri, Tevez alifikiria kustaafu soka kufuatia ugomvi wake na Kocha Mancini.

Kamanga na Matukio | 00:17 | 0 comments

Siku mbili baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu na nusu ambao utamuwezesha kuwepo Emirates Stadium hadi mwezi June mwaka 2016, mshambuliaji Theo Walcott ametoboa siri ya kukamilisha mpango huo.


Walcott ambae alizusha hofu kwa viongozi na mashabiki wa klabu ya Arsenal kutokana na kuonyesha hali ya kugomea mchakato wa kusaini mkataba huo mwanzoni mwa msimu huu, amesema siri kubwa ya kusaini mkataba mpya ni kutimizwa kwa matakwa yake ya kutaka kuchezeshwa kama mshambuliaji wa kati.


Amesema anaamini suala hilo litazingatiwa japo halitokua la kudumu, kutokana na mfumo utakaokuwa unatumiwa na meneja Arsene Wenger pale itakapohitajika kufanywa hivyo.


Naye, mshambuliaji kutoka nchini Argentina Carlos Tevez amesema alikaribia kufanya maamuzi ya kustahafu mchezo wa soka, kufuatia ugomvi wake na meneja wa klabu ya Man city Roberto Mancini uliojitokeza msimu uliopita.


Carlos Tevez mwenye umri wa miaka 28 amesema alikuwa katika mazingira magumu na wakati mwingine alidiriki kujifungia chumbani na kulia huku akujilaumu na kikitafsiri kitendo hicho kama mkosi uliokua umemkuta katika maisha yake ya soka.


Hata hivyo amesema alifikia maamuzi ya kujirekebisha yeye binafsi  kabla ya kuamua kurejea mjini Manchester na kuomba radhi kutokana na kosa alilolifanya na kisha kujiunga na wengine, hatua mbayo iliwasaidia wote kwa ujumla na kufanikisha azma ya kutwaa taji la Uingereza msimu uliopita.


Carlos Tevez alizusha sakata hilo, baada ya kugoma kupasha misuli moto wakati wa mchezo wa hatua ya makundi wa michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya FC Bayern Munich msimu uliopita.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger