Pages


Home » » Chama cha wendesha bajaji mkoani Mbeya kimetoa misaada mbalimbali katika kituo cha kulea watoto yatima.

Chama cha wendesha bajaji mkoani Mbeya kimetoa misaada mbalimbali katika kituo cha kulea watoto yatima.

Kamanga na Matukio | 02:42 | 0 comments

Mwenyekiti wa umoja Bajaji Mbeya Bw.Idd Ramadhan 
Chanzo:- Bomba FM 104.0MHz 
Chama cha wendesha bajaji  mkoani Mbeya kimetoa misaada mbalimbali katika  kituo  cha kulea watoto yatima  cha malezi na huruma kilichopo katika eneo la simike kwa lengo la kurudisha shukrani kwa wateja wake

Akizungumza na bomba fm mwenyekiti wa chama hicho  Idd Ramadhani amesema wamejiwekea mfumo wao kama chama cha bajaji kwa kufuata nyayo za mlenzi wa chama hicho Naibu Waziri wa Elimu Philipo Mulugo ili kuweza kuwasaidia wasiojiweza na kwamba kila wanajamii anapaswa kuguswa na kujitokeza kutoa misaada .  

Kwa upande wake katibu wa bajaji Ernest Mwaisangu  ameseviasa vikundi mbalimbali kuweza kujipanga na kuweza kutoa misaada kwa wasiojiweza  kuifahamisha serikali mambo muhimu ambayo yanafanyika katika kuisaidia jamii .

Kwa upande  Frank Musa mmoja wa  watoto hao  ametoa shkrani kwa chama hicho na kuwaomba kutokukata tama kuwasaidia ili nao waweze kuwasaidia wengine walitoa shukwani.

Aidha, kituo cha hicho kupitia mmoja wa walezi, kimetoa shukrani zake za dhati kwa umoja wa waendesha bajaji kwa kitendo cha kuwapatia misaada mbalimbali kituoni hapo.

Hata hivyo mdau mkuu wa umoja wa  wandesha bajaji hao Noah Mwakisu  vikundi vingine ili kuwapa hamasa zaidi na amevitaka vikundi vingine kuiga mfano kama huu waliouonyesha umoja wa bajaji  kwa kutoa misaada katika jamii
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger