Pages


Home » » Askari Polisi 7 wanatuhumiwa kwa kumpiga na kumjeruhi raia.

Askari Polisi 7 wanatuhumiwa kwa kumpiga na kumjeruhi raia.

Kamanga na Matukio | 02:46 | 0 comments
Na mwandishi wetu.
 Askari polisi saba wa kituo cha polisi Mbozi wanatuhumiwa kwa kumpiga, kumjeruhi na kumsababishia maumivu makali Laiton Mwakalinga mwenye umri wa miaka 33 mkazi wa Kijiji cha Haterere.



Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Laiton Mwakalinga alipigwa na askari wakati akipeleleka malalamiko dhidi ya shemeji yake aliyemtishia kumuua ambapo askari hao walimtaka atoe kiasi cha shilingi elfu arobaini na alipogoma ndipo walipoanza kumpiga hadi kumvunja mkono.



 Kutokana na kitendo hicho Kamanda wa polisi mkoani hapa Diwani Athumani ameahidi kulifuatilia tukio na kutoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa haraka na zenye ukweli ili tatizo kutafutiwa ufumbuzi ili kupatikana kwa haki sawa kwa raia na vyombo vya usalama.



Aidha amesema kitendo cha askari kumpiga raia ni kosa na halitakwi kufumbiwa macho na kwamba askari kuwakamata raia na  kuwapiga sio utaratibu na haipo katika utaratibu wa upelelezi wa jeshi hilo nani kosa la jinai na lisichukuliwe kama ni utaratibu wa Polisi bali ni wa mtu binafsi askari mmoja mmoja kujichukulia umamuzi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger