Pages


Home » » Chama cha madereva bajaji mkoani Mbeya kimedhamiria kurejesha shukrani zake kwa wateja

Chama cha madereva bajaji mkoani Mbeya kimedhamiria kurejesha shukrani zake kwa wateja

Kamanga na Matukio | 02:13 | 0 comments


Mwenyekiti wa umoja Bajaji mbeya Bw.Idd Ramadhan  

Chama cha madereva bajaji mkoani Mbeya kimedhamiria kurejesha shukrani zake kwa wateja wake kwa makundi maalum kwa kutoa misaada mbalimbali

Mwenyekiti wa chama hicho Idi Ramadhan amesema kwa kuanza chama hicho kitawatembelea watoto yatima katika kituo cha Isalaga kilicho Uyole Mbeya na zoezi hilo litafanyika kila mwisho wa mwezi.

Wakati huohuo amewataka vijana kuungana kwa pamoja katika kufanya kazi ikiwa ni pamoja na kuondokana na tabia ya kukaa vijuweni huku wakilalamika tatizo la ajira.

Aidha ameiomba Serikali kutimiza dhamira yake ya kusaidia vijana kwa vitendo ili waweze kuondokana na vitendo vya uhalifu na utumiaji wa dawa za kulevya.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger