Pages


Home » » TUKIWA BADO KATIKA UCHAGUZI WA TFF.

TUKIWA BADO KATIKA UCHAGUZI WA TFF.

Kamanga na Matukio | 01:26 | 0 comments
Bwana Fredrick Mwakalebela aliekua Katibu Mkuu wa TFF
 Aliekua katibu mkuu wa shirikisho la soka nchini TFF Fredrick Mwakalebela amezungumzia uchaguzi wa shirikisho hilo kwa kuitazama nafasi ya uraisi inayoonekana kutoa upinzani kwa Jamali Malinzi pamoja na Athumani Nyamlani ambae kwa sasa ni makamu wa kwanza wa raisi.

Mwakalebela ambae alitenda kazi zake kwa uadilifu mkubwa akiwa TFF kabla ya kutangaza kuaiacha nafasi ya ukatibu na kuingia katika masuala ya kisisa mwaka 2010, amesema licha ya kuwepo kwa mgombea  Omary Mussa Nkwarulo katika nafasi ya uraisi, bado anaona upinzani mkubwa bado upo kwa Jamali malinzi pamoja na Athumani Nyamlani.
 
Hata hivyo Fredrick Mwakalebeka akawataka wajumbe wa TFF kutumia nafasi yao ya kupiga kura kwa uadilifu mkubwa kutokana na hitaji la soka la bongo ambalo kwa sasa lina hamu ya kupata mafanikio kama ilivyo kwa nchi nyingi barani Afrika na kwingineko.


Wakati huo huo Uongozi wa chama chama cha makocha wa soka TAFCA mkoa wa umeyapokea kwa mikono miwili maamuzi ya kamati ya uchaguzi ya TFF ya kuuahirisha uchaguzi wa chama hicho taifa uliokua umepangwa kufanyika JAnuari 19 jijini Dar es salaa.

Katibu mkuu wa TAFCA Abubakari saidi Behengula amesema pamoja na maamuzi hayo kuchelewa kutplewa kwa wakati bado anaamini TAFCA itapata nafasi ya kujipanga upya na kufuata taratibu za kikatiba kwa ajili ya kukamilisha uchaguzi mkuu ambao umeamishwa kufanyika baada ya uchaguzi wa TFF.

Hata hivyo Saidi Behengula akaendelea kuzungumzia jambo linguine ambalo kwa upande wa Mwanza wameliona ni la busara zaidi baada ya kuutumia mkutano wa uchaguzi wa TAFCA kuwa kama mkutano mkuu wa kujadili agenda mbali mbali.

Amesema suala kubwa lillilomfurahisha ni kukubaliana kwa pamoja kuwa uongozi wa TAFCA taifa uliopo madarakani kupewa ridhaa ya kuendelea na kufuta kasumba ya kuunda kamati ya muda ya uongozi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger