Pages


Home » » UHABA WA MAFUTA MBEYA BAADHI YA WATEJA WAGOMEWA KUUZIWA MAFUTA HAYO.

UHABA WA MAFUTA MBEYA BAADHI YA WATEJA WAGOMEWA KUUZIWA MAFUTA HAYO.

Kamanga na Matukio | 06:36 | 0 comments
 Baadhi ya wateja wa mafuta wakiwa katika foleni katika kituo cha mafuta cha GAPCO kilichopo eneo la Mafiati jijini Mbeya kutokana na uhaba wa mafuta, hali iliyopelekea kuathiri shughuli mbalimbali za uzalishaji na usafirishaji kusimama na kupanda bei.
Dereva na Kondakta wa gari ya abiria maarufu daladala wakijadiliana jambo baada ya kugomewa kuuziwa mafuta pasipokuwa na sababu maalumu ambapo mtandao huu ulibaini kuwepo na ubaguzi katika uuzaji wa mafuta kutokana na kuangaliwa makampuni na umuhimu wa uhitaji kwa mteja.
*****
Habari na Mtandao huu.
Wamiliki wa vituo vya mafuta jijini Mbeya wameanza mgomo wa kuuza mafuta kuanzia jana majira ya saa tatu za usiku ambapo kituo kimoja cha BP ndicho kilichoonekana kuendelea kuuza mafuta jijini hapa.

Vituo hivyo vimefikia hatua ya kugoma kutoa huduma ya mafuta kwa jamii tangu mamlaka ya udhibiti wa nishati na madini (EWURA) itangaze kushusha bei ya mafuta aina ya Petroli kutoka shilingi elfu mbili mia moja kwa lita hadi kufikia shilingi elfu moja mia tisa themanini na tisa kwa sasa.

Kwa upande wake afisa habari wa EWURA bwana Taitus Kaguo amesema tatizo la mafuta kwa mikoa ya kanda ya nyanda za juu kusini inatokana na uharibifu wa miundombinu ya barabara eneo la kitonga ambayo inasababisha magari ya mizigo kushindwa kupita.

Wakati huohuo amesema katika kukabiliana na tatizo la migomo kwa miliki wa vituo vya mafuta kuanzia mwakani bei ya mafuta itakuwa ikipanda na kushukwa kila baada ya mwezi.

Naye meneja wa mamlaka ya usafiri wan chi kavu na maji SUMATRA mkoa wa Mbeya Amani Shamaje amewataka abiria kutoa taarifa kwa jeshi la polisi endapo nauli itapandishwa kutokana na kuwepo wka malalamiko kutoka kwa baadhi ya abiria kuwa nauli kutoka Mwanjelwa hadi Mbalizi kupanda kutoka shilingi mia tatu hamsini ya kawaida hadi kufikia shilingi mia tano.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger