Pages


Home » » ns: WANAFUNZI ELFU KUMI WASHINDWA KUCHAGULIWA KUJIUNGA NA MASOMO YA KIDATO CHA KWANZA MKOANI MBEYA

ns: WANAFUNZI ELFU KUMI WASHINDWA KUCHAGULIWA KUJIUNGA NA MASOMO YA KIDATO CHA KWANZA MKOANI MBEYA

Kamanga na Matukio | 02:58 | 0 comments
Wahitimu wa elimu ya msingi katika shule ya Msingi Kambarage iliyopo jijini Mbeya wakifurahia na kushangialia baada ya kumaliza kufanya mtihani wa darasa la saba ambao umemalizika na kuwapa fursa ya kusubiria Sherehe rasmi ya Kuangwa itakayofanyika wakati wowote kuanzia sasa. Wanafunzi wengi wameshangilia na kujawa furaha kubwa.,Je? furaha hii inaweza rudiwa tena wakati wa matokeo kutangazwa.
 *****
Habari na Picha na Mtandao huu.
Wanafunzi elfu kumi mia sita na saba waliohitimu elimu ya msingi mwaka huu mkoa wa Mbeya wameshindwa kuchaguliwa kujiunga na elimu ya Sekondari kutokana na uchache wa vyumba vya madarasa.

Hayo yamesemwa na afisa elimu mkoa wa Mbeya Juma Kaponda wakati akiongea na mwandishi wetu ofisini kwake na kuongeza kuwa waanafunzi hao watachaguliwa endapo ujenzi wa vyumba vya madarasa utakamilika.

Wakati huohuo amewataka wazazi kushiriki pia katika ujenzi wa ofisi ya utawala badala ya kujenga vyumba vya madarasa pekee.

Aidha Kaponda amesema kuwa wastani wa ufahulu umepanda kwa alama 13 kutoka 93 za mwaka 2009 hadi kufikia alama 106 ya mwaka 2011 ambao ni sawa na daraja la C.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger