Pages


Home » » TRA MKOANI MBEYA YAKABIDHI VYETI VYA ULIPAJI KODI BORA KWA TAASISI NA MASHARIKA.

TRA MKOANI MBEYA YAKABIDHI VYETI VYA ULIPAJI KODI BORA KWA TAASISI NA MASHARIKA.

Kamanga na Matukio | 05:30 | 0 comments
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Abbas Kandoro akimkabidhi cheti cha ulipaji kodi bora kutoka Mamlaka ya mapato nchini(TRA) kwa mkoa wa Mbeya, Meneja Mkuu wa Kituo cha Redio Bomba FM Bwana Kiyungi M. Kiyungi kilichopo mkoani hapa, ambapo  Taasisi na mashirika mengine yaliyokabidhi cheti cha ulipaji kodi bora ni pamoja na  Ofisi ya mkuu wa mkoa,  Acces Computer na Shule ya Sekondari Sangu.Zoezi la utoaji vyeti kwa Taasisi na Masharika limefanyika Kituo cha magari ya abiria(daladala) Kabwe jijini Mbeya.
Cheti cha ulipaji kodi bora kutoka Mamlaka ya mapato nchini (TRA) kwa mkoa wa Mbeya, kilichokabidhiwa kwa Kituo cha Redio Bomba FM kilichopo mkoani hapa, ambapo  Taasisi na mashirika mengine yaliyokabidhi cheti cha ulipaji kodi bora ni pamoja na  Ofisi ya mkuu wa mkoa,  Acces Computer na Shule ya Sekondari Sangu. Zoezi la utoaji vyeti kwa Taasisi na Masharika limefanyika Kituo cha magari ya abiria(daladala) Kabwe jijini Mbeya.
Walipa kodi bora kutoka Taasisi na mashirika yaliyokabidhi cheti cha ulipaji kodi bora ni Ofisi ya mkuu wa mkoa, kituo cha Redio Bomba fm Mbeya, Acces Computer na Sangu Sekondari, wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato nchini kwa mkoa wa Mbeya.  Zoezi la utoaji vyeti kwa Taasisi na Masharika limefanyika Kituo cha magari ya abiria(daladala) Kabwe jijini Mbeya.
 Kaimu Meneja wa Mamlaka ya mapato nchni(TRA) kwa mkoa wa Mbeya Bwana Sydney Mkamba(wa kwanza kushoto) katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Kituo cha redio Bomba FM baada ya kukabidhiwa cheti cha ulipaji bora wa kodi zoezi la utoaji vyeti kwa Taasisi na Masharika limefanyika Kituo cha magari ya abiria(daladala) Kabwe jijini Mbeya.
 Meneja wa Kituo cha redio Bomba FM Mbeya Bwana Kiyungi M. Kiyungi(wa kwanza kushoto), akifuatwiwa na Kaimu Meneja wa Mamlaka ya mapato nchni(TRA) kwa mkoa wa Mbeya Bwana Sydney Mkamba wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Kituo cha redio Bomba FM baada ya kukabidhiwa cheti cha ulipaji bora wa kodi zoezi la utoaji vyeti kwa Taasisi na Masharika limefanyika Kituo cha magari ya abiria(daladala) Kabwe jijini Mbeya.

HITIMISHO:-  Mamlaka ya mapato Tanzania mkoa wa Mbeya imekusanya zaidi ya shilingi bilioni 15 kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi juni hadi Septemba mwaka huu.

Akitoa pongezi kwa uongozi wa mamlaka ya mapato mkoani hapa mkuu wa mkoa wa Mbeya BASI KANDORO amesema maendeleo ya taifa huweza kupatikana kupitia kodi zinazolipwa na wafanyabiashara pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo wananachi wenyewe.

Aidha amezipongeza taasisi za Kiserikali, Zisizo za kiserikali, wafanyabiashara wadogo na wakubwa kwa kulipa kodi zao kila mwaka
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger