Pages


Home » » YALIYOJILI MKOANI MBEYA WIKI HILI

YALIYOJILI MKOANI MBEYA WIKI HILI

Kamanga na Matukio | 05:49 | 0 comments
 MISAADA:-Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abass Kadoro akikabidhi baadhi ya msaada kwa waathirika wa janga la mafuriko lililoathiri Kata ya Ikuti nje kidogo ya Jiji la Mbeya jana. Msaada hiyo ulikuwa ni pamoja na Blanketi 100,,Mikeka 100, Gunia 15 za mahindi na Lita 90 za mafuta. Kata hiyo ilikumbwa mafuriko ambapo zaidi ya kaya 30 zilikosa makazi ya kuishi.
 MISAADA:-Mkuu wa Wilaya Mbeya Evans Balama akikabidhi msaada wa Mchele, Mbuzi na Mafuta ya kula kwa watoto wa Gereza la watoto watukutu Jijini Meya jana kwa niaba ya rais Jakaya Kikwete ambaye ndiye aliyetoa msaada huo. (Picha na Ezekiel Kamanga).
 BAADA YA KUSHINDA KESI:- Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi akizungumza nje ya mahakama ya Mkoa wa Mbeya jana muda mfupi baada ya kufutiwa kwa kesi iliyokuwa ikimkabili ya kufanya mkutano kinyume cha Sheria. (Picha na Ezekiel Kamanga) 
 Mafuriko Mitaro:-Wakazi wa Kata ya Ikuti iliyopo nje kidogo ya Jiji la Mbeya wakirekebisha mtaro ambao uoliharibiwa vibaya na mafuriko yaliyoikumba Kata hiyo na kusababisha wakazi wa Kaya zaidi ya 30 kukosa makazi.
UFUNDI STADI:- Binti huyo pichani Happy Pius (9) ambaye ni mwanafunzi wa Shule ya Msingi Muungano ni mtoto mwenye kipaji cha pekee na kuwa kivutio kikubwa kwa wakazi wa Jiji la Mbeya kwa umahiri anaounesha kwa kutengeneza Pikipiki. Pichani Binti huyo akirekebisha moja ya Pikipiki iliyoletwa katika Gereji iliyopo eneo la Srereo Jijini Mbeya kama alivyokutwa na mpigapicha wetu jana.(Picha na Ezekiel Kamanga)  
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger