Pages


Home » » KANISA KATOLIKI JIMBO LA MBEYA LAINGIA DOSARI

KANISA KATOLIKI JIMBO LA MBEYA LAINGIA DOSARI

Kamanga na Matukio | 06:15 | 0 comments
Habari na Mtandao huu
Kanisa katoliki jimbo la Mbeya limeingia dosari baada ya Padri Inosent Sanga anayesimamia masuala ya elimu ya jimbo hilo kuwafukuza bila kulipa stahiki zao baadhi ya waalimu wa shule ya sekondari ya wasichana ya Mtakatifu Fransisko.

Licha ya padri Sanga kushindwa kuwa na ustahimilivu kwa watumishi wake hao pia alikaidi agizo la mahakama ambayo iliagiza watumishi hao kuendelea kuishi kwenye nyumba zinazomilikiwa na kanisa katoliki hadi hapo watakapo lipwa madai yao bada ya kufukuzwa kazi.

Waalimu hao waliondolewa vyombo vya nje na kampuni ya Yono Auction Mart and Cout Broker tawi la Mbeya amapo hata hivyo vyombo vya waalimu hao vilirudishwa ndani kwa nguvu na Serikali ya wilaya baada ya mkuu wa wilaya ya Mbeya Evansi Balama kufika eneo la tukio na kuzungumza na pande zote mbili.

Hata hivyo msemaji huyo wa shule ya senti frasisko padri Inosent Sanga aligoma kuzungumza lolote kwa waandishi wa habari.

Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amesema kuwa kitendo kilichofanywa na padri huyo si cha kiungwana na kwamba hakiendani na maadili ya mwenyezi Mungu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger