Pages


Home » » BEI ZA PEMBEJEO ZA KILIMO ZAPANDA KILA KUKICHA MKOANI MBEYA

BEI ZA PEMBEJEO ZA KILIMO ZAPANDA KILA KUKICHA MKOANI MBEYA

Kamanga na Matukio | 02:55 | 0 comments
Mifuko ya Mbolea aina ya DAP
*****
 Habari na Picha na Mtandao huu.
Licha ya Serikali kutunga sera yenye lengo la kumkomboa mkulima, Sera hiyo imeonekana kutokuwa na manufaa kwa wakulima kutokana na kupanda kwa bei za pembejeo za kila kila kukicha.

Wakiongea na mtandao huu baadhi ya wafanyabishara wa pembejeo za kilimo mji mdogo wa Mbalizi wilaya ya Mbeya vijijini wamesema kupanda kwa pembejeo hizo kunatokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji.

Mmoja wa wafanyabishara hao Bi.Atupele Mwakatima amesema bei ya Mbolea aina ya DAP walikuwa wakiiuza kwa shilingi elfu 37 ambapo sasa inauzwa shilingi elfu 75 Mbolea ya UREA ilikuwa ikiuzwa shilingi elfu 50 kwa sasa inauzwa shilingi elfu 65 na mbolea aina ya CAN ilikuwa ikiuzwa shilingi elfu 45 ambayo sasa inauzwa shilingi elfu 50.

Naye mmoja wa wakulima wilayani humo Bwana Fred LakimyoniI amesema kutokana na kupanda kwa gharama hizo za pembejeo kunauwezekano mkubwa wa bei ya mazao ikapanda mwakani ikiwa ni pamoja na baadhi ya wakulima kushindwa kulima kilimo bora kutokana na kushindwa kumudu gharama za kununulia pembejeo za kilimo. 
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger