Pages


Home » » Yaya Toure amemaliza mvutano na uongozi wa klabu ya Man City, baada ya kukubali kusaini mkataba wa mika minne.

Yaya Toure amemaliza mvutano na uongozi wa klabu ya Man City, baada ya kukubali kusaini mkataba wa mika minne.

Kamanga na Matukio | 02:32 | 0 comments
Na Shaban Kondo. Hatimae kiungo kutoka nchini Ivory Coast Yaya Toure amemaliza mvutano na uongozi wa klabu ya Man City, baada ya kukubali kusaini mkataba wa mika minne  ambao utamuwezesha kuendelea kuitumikia klabu hiyo ya mjini Manchester nchini Uingereza.


Taarifa zilizochapishwa katika mtandao wa klabu ya Man City zimeeleza kwamba mvutano uliokuwepo baina ya kiungo huyo mwenye umri wa miaka 29, haupo tena na sasa Yaya Toure ataendelea kuwepo Etihad kwa furaha na amani.


Taarifa hizo zimeeleza kubainisha kwamba mkataba wa miaka minne uliotiwa saini na mchezaji huyo ambae amekua muhimili mkubwa wa kikosi cha Roberto Mancini, utamuwezesha kulipwa kiasi cha paund million 11 kwa mwaka hatua mbayo imempandisha na kuwa miongoni mwa wachezaji wanaoendelea kulipwa mshahara mkubwa klabuni hapo.


Hata hivyo taarifa za Yaya Toure kuwa mbinu za kusaini mkataba mpya tayari zilikua zimeanza kuandikwa kwenye vyombo vya habari ambavyo vilimnukuu wakala wake Dimitri Seluk ambapo alidaiwa kuwaonya viongozi wa klabu ya Man City kuwa makini na suala la mchezaji wake na kama itakua kinyume na hapo huenda mwishoni mwa msimu huu angeanza kampeni ya kusaka klabu nyingine.


Kutokana na maelezo hayo ya wakala wa Yaya Toure, vyombo vya habari vilivyoandika taarifa hizo viliripoti kwamba uongozi wa Man City ulishtushwa na kauli hiyo na ndipo ulipoanza kufanya mipango ya haraka haraka ya kuhakikisha dili la kusianiwa kwa mkataba mpya linatimizwa kabla ya msimu huu haijafikia kikomo.


Wakati huo huo kiungo kutoka nchini Ufaransa, Samir Nasri amefungiwa kuendesha gari akiwa nchini Uingereza kwa muda wa miezi sita, baada ya kushindwa kulipa faini kutokana na kosa la kukutwa akiendesha gari kwa mwendokasi.


Samir Nasri ambae ni kiungo wa klabu ya Man City, ameangushiwa adhabu hiyo ikiwa ni baada ya siku moja ambapo mashabiki wa soka ulimwenguni kote kushuhudia ama kusikia adhabu iliyomuangukia Carlos Tevez ya kupewa siku 250 za kuhudumia jamii na pia kufungiwa miezi sita kwa kutokuwa na bima.


Nasri mwenye umri wa miaka 25 alipigwa faini ya paundi 1,900 lakini alifanikiwa kuiepuka baada ya kuandika barua kuwa hakujua kwamba gari lake aina ya Mercedes lilikuwa limekamatwa na kamera za barabarani kwa kosa la kwenda mwendokasi katika matukio matatu tofauti.


Hata hivyo Samir Nasri bado ana wigo wa kukata rufaa ya kupinga adhabu aliyopewa endapo ataona hakutendewa haki.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger