Pages


Home » » Cristiano Ronaldo amekanusha vikali tuhuma za kumsaliti rafiki yake wa kike Irina Shayk .

Cristiano Ronaldo amekanusha vikali tuhuma za kumsaliti rafiki yake wa kike Irina Shayk .

Kamanga na Matukio | 03:15 | 0 comments
Irina Shayk
 Mwanamitindo wa Brazil Andressa Urach ‘Miss BumBum’.


 Irina Shayk na Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo

Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo amekanusha vikali tuhuma za kumsaliti rafiki yake wa kike Irina Shayk kwa kutembea na mwanamitindo wa Brazil Andressa Urach ambaye anajulikana pia kwa jina ya ‘Miss BumBum’.


Urach alikaririwa na gazeti la The Sun akidai kuwa alilala na nyota huyo wa Madrid katika hoteli ya Villa Magna saa 48 kabla ya mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Dortmund lakini nyota huyo amesisitiza kuwa hakuna ukweli katika hilo.


Ronaldo aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa twitter akilalamikia kitendo cha mwanamitindo huyo kutaka kumchafua kwa kile kilichoandikwa katika gazeti hilo.


Ronaldo aliendelea kuandika kuwa ni kweli alifikia katika hoteli hiyo Aprili 22 kwa ajili ya mahojiano lakini mengine yote yaliyozungumza baada ya hapo ni uongo na uzushi mtupu
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger